Habari zinazotoka ndani ya Real Madrid zinaeleza kuwa Ferland Mendy anakabiliwa na kipindi kigumu zaidi katika maisha yake ya soka kutokana na matatizo ya majeraha yanayoendelea kumuandama. Beki huyo wa kushoto amecheza mechi tisa pekee msimu huu huku akipata majeraha matano tofauti, hali inayozidi kuongeza wasiwasi kuhusu mustakabali wake ndani ya mchezo.





