Harakati za usajili barani Ulaya zimeendelea kushika kasi huku vilabu vikubwa vikianza kupanga kikosi cha msimu ujao. Taarifa kutoka vyombo mbalimbali vya habari vya michezo vinaonyesha kuwa majina makubwa yanaweza kubadili klabu katika dirisha lijalo la majira ya kiangazi.




