Local,Simba, Lupopo, Transfer News

Simba yafuata mshambuliaji DR Congo

Joel JJ By Joel JJ
β€’
8 May 2026
Simba yafuata mshambuliaji DR Congo

Klabu ya Simba SC inaendelea kujiimarisha kuelekea msimu ujao, ambapo sasa imeelezwa kuwa inamfuatilia mshambuliaji wa klabu ya FC Saint-Γ‰loi Lupopo, Henoc Molia, anayesifika kwa kiwango bora katika Ligi Kuu ya DR Congo.

Taarifa zinaeleza kuwa Simba SC imeonyesha nia ya kumsajili Molia, ambaye kwa sasa anaichezea Lupopo na amekuwa mmoja wa wachezaji waliovutia zaidi msimu huu.

Mshambuliaji huyo ameonyesha kiwango cha juu akiwa amefunga mabao 13 na kutoa asisti 9, takwimu zinazomfanya kuwa miongoni mwa wachezaji hatari zaidi kwenye ligi hiyo.

Molia ambaye ana uwezo wa kucheza kama mshambuliaji wa kati au winga wa kushoto na kulia, alijiunga na Lupopo msimu uliopita akitokea AC Rangers, na sasa inaelezwa anafikiria changamoto mpya nje ya DR Congo.

Simba kufanya maboresho safu ya ushambuliaji

Simba SC inatarajiwa kufanya mabadiliko makubwa katika safu yake ya ushambuliaji kutokana na kutokuwepo kwa uthabiti wa mabao katika michezo ya karibuni.

Kocha mkuu wa Simba, Steve Barker, amekuwa akilazimika kubadilisha mfumo wa timu mara kadhaa akicheza bila mshambuliaji wa asili katika baadhi ya mechi.

Kwa sasa, ni Suleiman Mwalimu pekee anayetegemewa sana katika nafasi hiyo, ingawa naye yupo kwa mkopo na mustakabali wake bado haujafahamika wazi.

Inaelezwa kuwa Mwalimu anaweza kurejea katika klabu yake ya Wydad AC endapo makubaliano mapya hayatafikiwa kati ya pande zote mbili.

Hatma ya Jonathan Sowah ndani ya Simba

Wakati huo huo, mshambuliaji kutoka Ghana, Jonathan Sowah, naye anaonekana kuwa katika wakati mgumu baada ya kuingia kwenye mtafaruko na viongozi wa Simba.

Inaelezwa kuwa licha ya kuagizwa kufanya mazoezi na kikosi cha vijana, Sowah amegoma kufanya hivyo hali inayozidi kuashiria uwezekano wa kuondoka klabuni hapo.

Uongozi wa Simba SC unaonekana kutafuta suluhisho la muda mrefu katika safu ya ushambuliaji ili kuhakikisha timu inakuwa na uwiano mzuri wa mabao msimu ujao.

More Stories

Barcelona yaendeleza kichapo Laliga ikimfunga Sevilla, Raphinha hashikiki.
Barcelona yaendeleza kichapo Laliga ikimfunga Sevilla, Raphinha hashikiki.
5h ago
READ MORE β†’
Mamelodi Sundowns yaibuka kidedea mbele ya Al Ahli
Mamelodi Sundowns yaibuka kidedea mbele ya Al Ahli
9h ago
READ MORE β†’
Arsenal yaduwazwa 3-0 na Brighton
Arsenal yaduwazwa 3-0 na Brighton
10h ago
READ MORE β†’
Nyota Stars waingia kambini tayari kwa mechi za kufuzu Afcon 2027
Nyota Stars waingia kambini tayari kwa mechi za kufuzu Afcon 2027
12h ago
READ MORE β†’
Simba kujichimbia Afrika Kusini kujiandaa na Kariakoo Derby
Simba kujichimbia Afrika Kusini kujiandaa na Kariakoo Derby
12h ago
READ MORE β†’
Madrid Derby: Atletico na Real kwenye vita ya majirani
Madrid Derby: Atletico na Real kwenye vita ya majirani
16h ago
READ MORE β†’
Hii hapa rekodi tamu ya Barker Ligi Kuu
Hii hapa rekodi tamu ya Barker Ligi Kuu
18h ago
READ MORE β†’
Sundowns kuchuana na Al Ahli katika vita ya Afrika na Asia
Sundowns kuchuana na Al Ahli katika vita ya Afrika na Asia
18h ago
READ MORE β†’
Ft: Yanga 1-0 St George, Yanga yapata ushindi mechi ya kirafiki.
Ft: Yanga 1-0 St George, Yanga yapata ushindi mechi ya kirafiki.
1d ago
READ MORE β†’
Dockers Derby yarudi baada ya miaka 14, Ulinzi wa London ukiimarishwa.
Dockers Derby yarudi baada ya miaka 14, Ulinzi wa London ukiimarishwa.
1d ago
READ MORE β†’