Local,Normal News,Azam, TRA

Sintofahamu kuugua ghafla kwa wachezaji Azam Fc

Joel JJ By Joel JJ
β€’
10 May 2026
Sintofahamu kuugua ghafla kwa wachezaji Azam Fc

Wachezaji saba wa klabu ya Azam wameripotiwa kupata maumivu makali ya tumbo na kichwa ambapo wengi wao wamekimbizwa hospital ili kupatiwa matibabu.

Taarifa za awali zinaeleza kuwa baadhi ya nyota wa kikosi hicho walionyesha dalili za kutokuwa sawa kiafya hali iliyowalazimu kupata uangalizi wa karibu kutoka kwa madaktari wa timu huku nyota Ashraf kibeku akidai alianza kuhisi vibaya mnamo dakika ya 20 wakati mechi yao na TRA inaendelea.

Wachezaji wengine ambao wameripotiwa kukumbwa na shida ya kiafya ni pamoja na Faisal Salum, Lusajo Mwaikenda na Pascal Msindo ambaye pia inaelezwa anapata shida kwenye kupumua na kooni kwake.

Hata hivyo hakuna taarifa rasmi kutoka uongozi wa Azam FC kuhusu chanzo cha hali hiyo wala ukubwa wa tatizo hilo.

More Stories

Nyota Geita Gold afunguka rafu ya Aziz KI, Ilikuwa bahati mbaya
Nyota Geita Gold afunguka rafu ya Aziz KI, Ilikuwa bahati mbaya
4h ago
READ MORE β†’
LAPORTA: Atletico kumuuza Alvarez kwa timu yeyote isipokuwa Barcelona
LAPORTA: Atletico kumuuza Alvarez kwa timu yeyote isipokuwa Barcelona
6h ago
READ MORE β†’
Ngorongoro Heroes yatangulia nusu fainali CECAFA U20 kwa kishindo
Ngorongoro Heroes yatangulia nusu fainali CECAFA U20 kwa kishindo
8h ago
READ MORE β†’
Samatta afunga bao lake la pili, Le Havre ikipoteza
Samatta afunga bao lake la pili, Le Havre ikipoteza
8h ago
READ MORE β†’
Salah hakamatiki Uturuki, apiga hat-trik Trabzonspor ikiifumua Galatasaray 4-0
Salah hakamatiki Uturuki, apiga hat-trik Trabzonspor ikiifumua Galatasaray 4-0
9h ago
READ MORE β†’
Azam Fc yaonywa, Yanga yakumbana na faini - Kamati ya saa 72
Azam Fc yaonywa, Yanga yakumbana na faini - Kamati ya saa 72
9h ago
READ MORE β†’
Mshambuliaji wa zamani Yanga aibukia Zambia
Mshambuliaji wa zamani Yanga aibukia Zambia
10h ago
READ MORE β†’
Barcelona yaendeleza kichapo Laliga ikimfunga Sevilla, Raphinha hashikiki.
Barcelona yaendeleza kichapo Laliga ikimfunga Sevilla, Raphinha hashikiki.
17h ago
READ MORE β†’
Mamelodi Sundowns yaibuka kidedea mbele ya Al Ahli
Mamelodi Sundowns yaibuka kidedea mbele ya Al Ahli
22h ago
READ MORE β†’
Arsenal yaduwazwa 3-0 na Brighton
Arsenal yaduwazwa 3-0 na Brighton
22h ago
READ MORE β†’