Kamwe ahoji Yanga kukosa tuzo BMT

Joel JJ By Joel JJ β€’ 11th May 2026


Kamwe ahoji Yanga kukosa tuzo BMT

Juzi klabu ya Simba ilishinda tuzo ya timu bora ya Mwaka 2025 tuzo zilizotolewa na Baraza la Michezo la Taifa (BMT) kwa Taasisi na watu waliofanya vyema mwaka 2025.

Simba ilishinda tuzo hiyo baada ya kufika fainali ya kombe la Shirikisho mwaka 2025.

Hata hivyo tuzo hiyo ikamuibua Meneja wa Habari na Mawasiliano wa Yanga Ali Kamwe akihoji vigezo vilivyotumika kuipa Simba tuzo hiyo.

Kupitia ukurasa wake wa mtandao wa kijamii, Kamwe alikumbusha namna mwaka 2023 Yanga ilivyotwaa tuzo hiyo kwa kuzingatia mafanikio kadhaa makubwa yaliyopatikana ndani na nje ya nchi.

Kwa mujibu wa Kamwe, mwaka huo Yanga ilipewa tuzo kutokana na:

  • Kufika Fainali ya Kombe la Shirikisho Afrika (CAFCC)
  • Kutwaa Ubingwa wa Ligi Kuu Tanzania Bara
  • Kushinda Kombe la Shirikisho la Azam

Kamwe ameonyesha kushangazwa na kile alichodai kuwa ni mabadiliko ya ghafla ya vigezo vya utoaji wa tuzo hizo.

β€œMwaka 2023 sababu zilielezwa wazi kabisa mbele ya wadau wote. Leo tunaambiwa hatuna elimu na hatujui vigezo,” alihoji Kamwe.

Aidha, Kamwe amesema hali hiyo inaonyesha kuwa mafanikio ya ndani kama ubingwa wa ligi na makombe ya nyumbani hayapewi uzito mkubwa mbele ya mafanikio ya kufika hatua za mwisho katika michuano ya kimataifa.

Msimu uliopita Yanga ilitwaa mataji yote ya ndani yaani Ngao ya Jamii, Ligi Kuu, kombe la Mapinduzi, kombe la Muungano na kombe la CRDB lakini mataji hayo hayajatosha kwa Wananchi kushinda tuzo hiyo mbele ya watani zao Simba waliomaliza msimu mafanikio pekee yakiwa kucheza fainali ya CAFCC


  

More Stories

Azam Fc hiyooo fainali, yaichapa Yanga 3-2 nusu fainali
Azam Fc hiyooo fainali, yaichapa Yanga 3-2 nusu fainali
Today, READ MORE β†’
Azam Fc 3-2 Yanga, CRDB Cup
Azam Fc 3-2 Yanga, CRDB Cup
Today, READ MORE β†’
Ni Azam Fc vs Yanga, nani anakwenda fainali kombe la CRDB?
Ni Azam Fc vs Yanga, nani anakwenda fainali kombe la CRDB?
Today, READ MORE β†’
Liverpool kuongeza dau kumnasa Diomande
Liverpool kuongeza dau kumnasa Diomande
Today, READ MORE β†’
Prisons wamefufua matumaini kusalia ligi kuu
Prisons wamefufua matumaini kusalia ligi kuu
Today, READ MORE β†’
Tunisia yaaga kombe la Dunia kwa aibu, yapigwa 4-0 na Japan
Tunisia yaaga kombe la Dunia kwa aibu, yapigwa 4-0 na Japan
Today, READ MORE β†’
Ivory Coast yapoteza dhidi ya Ujerumani dakika za jioni
Ivory Coast yapoteza dhidi ya Ujerumani dakika za jioni
Today, READ MORE β†’
Real Madrid yakana kuwasiliana na Olise, wakala wake
Real Madrid yakana kuwasiliana na Olise, wakala wake
Yesterday, READ MORE β†’
Simba 4-0 Coastal Union, CRDB Cup
Simba 4-0 Coastal Union, CRDB Cup
Yesterday, READ MORE β†’
Simba yaifumua Coastal Union 4-0, yatinga fainali ya CRDB Bank Cup
Simba yaifumua Coastal Union 4-0, yatinga fainali ya CRDB Bank Cup
Yesterday, READ MORE β†’