Local,Normal News,Yanga, Simba, BMT

Kamwe ahoji Yanga kukosa tuzo BMT

Joel JJ By Joel JJ
11 May 2026
Kamwe ahoji Yanga kukosa tuzo BMT

Juzi klabu ya Simba ilishinda tuzo ya timu bora ya Mwaka 2025 tuzo zilizotolewa na Baraza la Michezo la Taifa (BMT) kwa Taasisi na watu waliofanya vyema mwaka 2025.

Simba ilishinda tuzo hiyo baada ya kufika fainali ya kombe la Shirikisho mwaka 2025.

Hata hivyo tuzo hiyo ikamuibua Meneja wa Habari na Mawasiliano wa Yanga Ali Kamwe akihoji vigezo vilivyotumika kuipa Simba tuzo hiyo.

Kupitia ukurasa wake wa mtandao wa kijamii, Kamwe alikumbusha namna mwaka 2023 Yanga ilivyotwaa tuzo hiyo kwa kuzingatia mafanikio kadhaa makubwa yaliyopatikana ndani na nje ya nchi.

Kwa mujibu wa Kamwe, mwaka huo Yanga ilipewa tuzo kutokana na:

  • Kufika Fainali ya Kombe la Shirikisho Afrika (CAFCC)
  • Kutwaa Ubingwa wa Ligi Kuu Tanzania Bara
  • Kushinda Kombe la Shirikisho la Azam

Kamwe ameonyesha kushangazwa na kile alichodai kuwa ni mabadiliko ya ghafla ya vigezo vya utoaji wa tuzo hizo.

“Mwaka 2023 sababu zilielezwa wazi kabisa mbele ya wadau wote. Leo tunaambiwa hatuna elimu na hatujui vigezo,” alihoji Kamwe.

Aidha, Kamwe amesema hali hiyo inaonyesha kuwa mafanikio ya ndani kama ubingwa wa ligi na makombe ya nyumbani hayapewi uzito mkubwa mbele ya mafanikio ya kufika hatua za mwisho katika michuano ya kimataifa.

Msimu uliopita Yanga ilitwaa mataji yote ya ndani yaani Ngao ya Jamii, Ligi Kuu, kombe la Mapinduzi, kombe la Muungano na kombe la CRDB lakini mataji hayo hayajatosha kwa Wananchi kushinda tuzo hiyo mbele ya watani zao Simba waliomaliza msimu mafanikio pekee yakiwa kucheza fainali ya CAFCC

More Stories

APR Fc yawaondosha aigles du congo kwenye caf champions league
APR Fc yawaondosha aigles du congo kwenye caf champions league
5h ago
READ MORE →
Azam Fc yaomboleza kifo cha mlinda lango U20
Azam Fc yaomboleza kifo cha mlinda lango U20
8h ago
READ MORE →
Hatuna presha kuikabili Yanga - Kocha Gaborone United
Hatuna presha kuikabili Yanga - Kocha Gaborone United
10h ago
READ MORE →
Manqoba aweka tahadhari mechi dhidi ya Gaborone United
Manqoba aweka tahadhari mechi dhidi ya Gaborone United
12h ago
READ MORE →
Rasmi: João Pedro Atwaa Tuzo Ya Mchezaji Bora Wa Mwezi Wa Agosti
Rasmi: João Pedro Atwaa Tuzo Ya Mchezaji Bora Wa Mwezi Wa Agosti
14h ago
READ MORE →
Simba inalenga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, nusu fainali ni lengo kubwa
Simba inalenga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, nusu fainali ni lengo kubwa
15h ago
READ MORE →
Libasse awapiga chini Max na Mwajanga, Kwenye tuzo za Mwezi.
Libasse awapiga chini Max na Mwajanga, Kwenye tuzo za Mwezi.
15h ago
READ MORE →
Fei Toto azipotezea Simba, Yanga
Fei Toto azipotezea Simba, Yanga
17h ago
READ MORE →
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 21, Septemba 11 2026
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 21, Septemba 11 2026
20h ago
READ MORE →
UEFA champions league: matokeo ya usiku
UEFA champions league: matokeo ya usiku
1d ago
READ MORE →