Chama anakusanya tuzo tu

Joel JJ By Joel JJ • 11th May 2026


Chama anakusanya tuzo tu

Kiungo mshambuliaji wa Simba SC, Clatous Chama maarufu kama ‘Mwamba wa Lusaka’, ameendelea kudhihirisha kiwango chake bora ndani ya kikosi hicho baada ya kutwaa tuzo ya nyota wa mchezo katika mechi tatu mfululizo.

Nyota huyo raia wa Zambia ameonyesha kuwa ni mhimili mkubwa wa mafanikio ya Simba katika michezo ya hivi karibuni, akihusika moja kwa moja kwenye mabao muhimu yaliyoiwezesha timu yake kuendelea kufanya vizuri kwenye Ligi Kuu Tanzania Bara.

Jana, akiiongoza Simba kuibuka na ushindi mnono wa mabao 4-0 dhidi ya Tanzania Prisons, Chama alifunga bao moja na kutoa pasi ya usaidizi wa bao jingine, jambo lililomfanya aondoke tena na tuzo ya Man of the Match.

Mwamba huyo wa Lusaka sasa amefunga katika mechi tatu mfululizo huku kila mchezo akiondoka na tuzo ya mchezaji bora wa mechi.

Mnamo Mei 03, kwenye dabi kali dhidi ya Yanga iliyomalizika kwa sare ya mabao 2-2, Chama aling’ara kwa kufunga bao na kutoa pasi ya bao kabla ya kutwaa tuzo ya nyota wa mchezo baada ya dakika 90 kukamilika.

Baadaye Mei 06, katika mchezo dhidi ya JKT Tanzania uliochezwa Dimba la Meja Jenerali Isamuhyo, kiungo huyo alifunga bao pekee lililoipa Simba ushindi wa bao 1-0 na pointi tatu muhimu, huku akichukua tena tuzo ya mchezaji bora wa mechi.

Dhidi ya Prisons jana, Chama alifikisha mabao sita msimu huu sambamba na asisti nne tangu kurejea kwake Msimbazi katika dirisha dogo la usajili.

Tangu arejee ndani ya kikosi cha Simba, Chama tayari ametwaa jumla ya tuzo tano za nyota wa mchezo, ishara ya kiwango chake kikubwa na mchango wake ndani ya timu hiyo.


  

More Stories

Azam Fc hiyooo fainali, yaichapa Yanga 3-2 nusu fainali
Azam Fc hiyooo fainali, yaichapa Yanga 3-2 nusu fainali
Today, READ MORE →
Azam Fc 3-2 Yanga, CRDB Cup
Azam Fc 3-2 Yanga, CRDB Cup
Today, READ MORE →
Ni Azam Fc vs Yanga, nani anakwenda fainali kombe la CRDB?
Ni Azam Fc vs Yanga, nani anakwenda fainali kombe la CRDB?
Today, READ MORE →
Liverpool kuongeza dau kumnasa Diomande
Liverpool kuongeza dau kumnasa Diomande
Today, READ MORE →
Prisons wamefufua matumaini kusalia ligi kuu
Prisons wamefufua matumaini kusalia ligi kuu
Today, READ MORE →
Tunisia yaaga kombe la Dunia kwa aibu, yapigwa 4-0 na Japan
Tunisia yaaga kombe la Dunia kwa aibu, yapigwa 4-0 na Japan
Today, READ MORE →
Ivory Coast yapoteza dhidi ya Ujerumani dakika za jioni
Ivory Coast yapoteza dhidi ya Ujerumani dakika za jioni
Today, READ MORE →
Real Madrid yakana kuwasiliana na Olise, wakala wake
Real Madrid yakana kuwasiliana na Olise, wakala wake
Yesterday, READ MORE →
Simba 4-0 Coastal Union, CRDB Cup
Simba 4-0 Coastal Union, CRDB Cup
Yesterday, READ MORE →
Simba yaifumua Coastal Union 4-0, yatinga fainali ya CRDB Bank Cup
Simba yaifumua Coastal Union 4-0, yatinga fainali ya CRDB Bank Cup
Yesterday, READ MORE →