Local,Normal News,Simba

Chama anakusanya tuzo tu

Joel JJ By Joel JJ
11 May 2026
Chama anakusanya tuzo tu

Kiungo mshambuliaji wa Simba SC, Clatous Chama maarufu kama ‘Mwamba wa Lusaka’, ameendelea kudhihirisha kiwango chake bora ndani ya kikosi hicho baada ya kutwaa tuzo ya nyota wa mchezo katika mechi tatu mfululizo.

Nyota huyo raia wa Zambia ameonyesha kuwa ni mhimili mkubwa wa mafanikio ya Simba katika michezo ya hivi karibuni, akihusika moja kwa moja kwenye mabao muhimu yaliyoiwezesha timu yake kuendelea kufanya vizuri kwenye Ligi Kuu Tanzania Bara.

Jana, akiiongoza Simba kuibuka na ushindi mnono wa mabao 4-0 dhidi ya Tanzania Prisons, Chama alifunga bao moja na kutoa pasi ya usaidizi wa bao jingine, jambo lililomfanya aondoke tena na tuzo ya Man of the Match.

Mwamba huyo wa Lusaka sasa amefunga katika mechi tatu mfululizo huku kila mchezo akiondoka na tuzo ya mchezaji bora wa mechi.

Mnamo Mei 03, kwenye dabi kali dhidi ya Yanga iliyomalizika kwa sare ya mabao 2-2, Chama aling’ara kwa kufunga bao na kutoa pasi ya bao kabla ya kutwaa tuzo ya nyota wa mchezo baada ya dakika 90 kukamilika.

Baadaye Mei 06, katika mchezo dhidi ya JKT Tanzania uliochezwa Dimba la Meja Jenerali Isamuhyo, kiungo huyo alifunga bao pekee lililoipa Simba ushindi wa bao 1-0 na pointi tatu muhimu, huku akichukua tena tuzo ya mchezaji bora wa mechi.

Dhidi ya Prisons jana, Chama alifikisha mabao sita msimu huu sambamba na asisti nne tangu kurejea kwake Msimbazi katika dirisha dogo la usajili.

Tangu arejee ndani ya kikosi cha Simba, Chama tayari ametwaa jumla ya tuzo tano za nyota wa mchezo, ishara ya kiwango chake kikubwa na mchango wake ndani ya timu hiyo.

More Stories

Manchester City yaichapa Sunderland 5–3 katika mechi ya mabao nane
Manchester City yaichapa Sunderland 5–3 katika mechi ya mabao nane
2h ago
READ MORE →
Atletico yang’ara kwenye dabi, Real Madrid aangukia pua ugenini
Atletico yang’ara kwenye dabi, Real Madrid aangukia pua ugenini
3h ago
READ MORE →
Nyota Geita Gold afunguka rafu ya Aziz KI, Ilikuwa bahati mbaya
Nyota Geita Gold afunguka rafu ya Aziz KI, Ilikuwa bahati mbaya
8h ago
READ MORE →
LAPORTA: Atletico kumuuza Alvarez kwa timu yeyote isipokuwa Barcelona
LAPORTA: Atletico kumuuza Alvarez kwa timu yeyote isipokuwa Barcelona
10h ago
READ MORE →
Ngorongoro Heroes yatangulia nusu fainali CECAFA U20 kwa kishindo
Ngorongoro Heroes yatangulia nusu fainali CECAFA U20 kwa kishindo
13h ago
READ MORE →
Samatta afunga bao lake la pili, Le Havre ikipoteza
Samatta afunga bao lake la pili, Le Havre ikipoteza
13h ago
READ MORE →
Salah hakamatiki Uturuki, apiga hat-trik Trabzonspor ikiifumua Galatasaray 4-0
Salah hakamatiki Uturuki, apiga hat-trik Trabzonspor ikiifumua Galatasaray 4-0
13h ago
READ MORE →
Azam Fc yaonywa, Yanga yakumbana na faini - Kamati ya saa 72
Azam Fc yaonywa, Yanga yakumbana na faini - Kamati ya saa 72
14h ago
READ MORE →
Mshambuliaji wa zamani Yanga aibukia Zambia
Mshambuliaji wa zamani Yanga aibukia Zambia
14h ago
READ MORE →
Barcelona yaendeleza kichapo Laliga ikimfunga Sevilla, Raphinha hashikiki.
Barcelona yaendeleza kichapo Laliga ikimfunga Sevilla, Raphinha hashikiki.
22h ago
READ MORE →