Local,Normal News,Yanga, Dodoma

Yanga yakumbana na rungu la Kamati ya saa 72

Joel JJ By Joel JJ
β€’
11 May 2026
Yanga yakumbana na rungu la Kamati ya saa 72

Maamuzi ya Kamati ya Uendeshaji na Usimamizi wa Ligi ya Bodi ya Ligi Kuu Tanzania (TPLB) kufuatia kikao cha tarehe 9 Mei, 2026:


1. Ligi Kuu ya NBC

Mechi: Simba SC 2-2 Young Africans (Mechi Na. 169)

Kamati imetoa adhabu kadhaa kwa klabu ya Yanga kufuatia mchezo huu uliopigwa Mei 3, 2026:

  • Kuchelewa kufika uwanjani: Klabu imepewa Onyo Kali kwa kufika uwanjani saa 10:35 alasiri badala ya saa 10:30 alasiri.

  • Kususia chumba cha kuvalia: Klabu imetozwa faini ya Sh. 30,000,000 (milioni thelathini). Wachezaji na maofisa walikataa kutumia chumba rasmi cha kuvalia katika Uwanja wa Meja Jenerali Isamuhyo na badala yake walitumia nyumba iliyo nje ya uwanja.

  • Meneja Walter Harson: Amefungiwa michezo mitatu na kupigwa faini ya Sh. 1,000,000 (milioni moja) kwa kosa la kumsukuma mchezaji wa Simba, Clatous Chama.

  • Shabiki Mohamed Ally Mposo: Amefungiwa kuingia uwanjani kwa miezi 12 kwa kosa la kuingia uwanjani wakati wa mapumziko na kumwaga vimiminika (vitendo vinavyotafsiriwa kama imani za kishirikina).

Mechi: Mtibwa Sugar 0-1 Dodoma Jiji FC (Mechi Na. 154)

  • Dodoma Jiji FC: Imetozwa faini ya Sh. 5,000,000 (milioni tano) kwa kuchelewa kufika kwenye kikao cha maandalizi ya mchezo (MCM) na kufika wakiwa pungufu ya vifaa na wawakilishi wanaohitajika kikanuni.

More Stories

Barcelona yaendeleza kichapo Laliga ikimfunga Sevilla, Raphinha hashikiki.
Barcelona yaendeleza kichapo Laliga ikimfunga Sevilla, Raphinha hashikiki.
5h ago
READ MORE β†’
Mamelodi Sundowns yaibuka kidedea mbele ya Al Ahli
Mamelodi Sundowns yaibuka kidedea mbele ya Al Ahli
10h ago
READ MORE β†’
Arsenal yaduwazwa 3-0 na Brighton
Arsenal yaduwazwa 3-0 na Brighton
10h ago
READ MORE β†’
Nyota Stars waingia kambini tayari kwa mechi za kufuzu Afcon 2027
Nyota Stars waingia kambini tayari kwa mechi za kufuzu Afcon 2027
12h ago
READ MORE β†’
Simba kujichimbia Afrika Kusini kujiandaa na Kariakoo Derby
Simba kujichimbia Afrika Kusini kujiandaa na Kariakoo Derby
13h ago
READ MORE β†’
Madrid Derby: Atletico na Real kwenye vita ya majirani
Madrid Derby: Atletico na Real kwenye vita ya majirani
16h ago
READ MORE β†’
Hii hapa rekodi tamu ya Barker Ligi Kuu
Hii hapa rekodi tamu ya Barker Ligi Kuu
18h ago
READ MORE β†’
Sundowns kuchuana na Al Ahli katika vita ya Afrika na Asia
Sundowns kuchuana na Al Ahli katika vita ya Afrika na Asia
19h ago
READ MORE β†’
Ft: Yanga 1-0 St George, Yanga yapata ushindi mechi ya kirafiki.
Ft: Yanga 1-0 St George, Yanga yapata ushindi mechi ya kirafiki.
1d ago
READ MORE β†’
Dockers Derby yarudi baada ya miaka 14, Ulinzi wa London ukiimarishwa.
Dockers Derby yarudi baada ya miaka 14, Ulinzi wa London ukiimarishwa.
1d ago
READ MORE β†’