Kocha Mkuu wa Tanzania Prisons, Shadrack Nsajigwa bado anaendelea kusaka ushindi wake wa kwanza katika Ligi Kuu NBC Tanzania Bara tangu ajiunge na kikosi hicho.
Nsajigwa ambaye aliwahi kuwa nahodha wa Yanga ameiongoza Tanzania Prisons katika michezo tisa ya ligi kuu bila kupata ushindi hata mmoja, hali inayozidi kuongeza presha ndani ya timu hiyo.





