International,Transfer News,Real Madrid, Local

Mourinho ni suala la muda tu Real Madrid

Joel JJ By Joel JJ
11 May 2026
Mourinho ni suala la muda tu Real Madrid

Taarifa zinazidi kushika kasi barani Ulaya kuhusu uwezekano wa kocha José Mourinho kurejea ndani ya Real Madrid kwa mara nyingine.

Licha ya Mourinho kujitokeza hadharani na kukanusha kufanya mazungumzo yoyote na viongozi wa Madrid, ripoti mbalimbali kutoka Hispania na Ureno zinaeleza kuwa mawasiliano ya chini kwa chini bado yanaendelea.

Vyombo kadhaa vya habari Ulaya vimeripoti kuwa Rais wa Real Madrid, Florentino Pérez anamtazama Mourinho kama chaguo sahihi la kurejesha nidhamu na ushindani ndani ya kikosi hicho baada ya msimu wenye matokeo yasiyoridhisha.

Mourinho ambaye kwa sasa anaifundisha Benfica, amekuwa akihusishwa vikali na kurejea Santiago Bernabéu, huku baadhi ya ripoti zikidai kuwa tayari viongozi wa Benfica wameanza kutafuta mbadala wake endapo dili hilo litakamilika.

Katika mkutano wake wa hivi karibuni na waandishi wa habari, Mourinho alisema bado hajapigiwa simu na mtu yeyote kutoka Real Madrid na kwamba ataendelea kubaki makini na majukumu yake Benfica hadi mwisho wa msimu.

Hata hivyo, ripoti nyingine zinaeleza kuwa nyuma ya pazia tayari kuna majadiliano yanayoendelea kuhusu uwezekano wa Mourinho kurejea Bernabéu, huku Perez akitajwa kuwa mtu mwenye ushawishi mkubwa kwenye uamuzi huo.

Mourinho aliwahi kuifundisha Real Madrid kati ya mwaka 2010 hadi 2013 ambapo aliipa ubingwa wa La Liga, Copa del Rey pamoja na kuiwezesha kurejea kuwa tishio Ulaya. Kipindi chake kilikumbukwa zaidi kwa ushindani mkubwa dhidi ya FC Barcelona ya wakati huo chini ya Pep Guardiola.

More Stories

APR Fc yawaondosha aigles du congo kwenye caf champions league
APR Fc yawaondosha aigles du congo kwenye caf champions league
6m ago
READ MORE →
Azam Fc yaomboleza kifo cha mlinda lango U20
Azam Fc yaomboleza kifo cha mlinda lango U20
3h ago
READ MORE →
Hatuna presha kuikabili Yanga - Kocha Gaborone United
Hatuna presha kuikabili Yanga - Kocha Gaborone United
5h ago
READ MORE →
Manqoba aweka tahadhari mechi dhidi ya Gaborone United
Manqoba aweka tahadhari mechi dhidi ya Gaborone United
7h ago
READ MORE →
Rasmi: João Pedro Atwaa Tuzo Ya Mchezaji Bora Wa Mwezi Wa Agosti
Rasmi: João Pedro Atwaa Tuzo Ya Mchezaji Bora Wa Mwezi Wa Agosti
9h ago
READ MORE →
Simba inalenga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, nusu fainali ni lengo kubwa
Simba inalenga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, nusu fainali ni lengo kubwa
10h ago
READ MORE →
Libasse awapiga chini Max na Mwajanga, Kwenye tuzo za Mwezi.
Libasse awapiga chini Max na Mwajanga, Kwenye tuzo za Mwezi.
10h ago
READ MORE →
Fei Toto azipotezea Simba, Yanga
Fei Toto azipotezea Simba, Yanga
12h ago
READ MORE →
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 21, Septemba 11 2026
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 21, Septemba 11 2026
15h ago
READ MORE →
UEFA champions league: matokeo ya usiku
UEFA champions league: matokeo ya usiku
22h ago
READ MORE →