International,Normal News,Real Madrid, Local

Perez asisitiza haumwi, yuko fit kuiongoza Real Madrid

Joel JJ By Joel JJ
12 May 2026
Perez asisitiza haumwi, yuko fit kuiongoza Real Madrid

Rais wa Real Madrid Florentino Perez, ameweka wazi kuwa hana mpango wa kujiuzulu na badala yake atagombea tena nafasi ya urais wa klabu hiyo kubwa ya Hispania.

Akizungumza katika mkutano wa dharura na wanahabari uliofanyika leo Jumanne, Mei 12, 2026, Pérez alisema kuwa kuna kampeni maalum inayolenga kumchafua na kuivuruga Real Madrid, hasa baada ya klabu hiyo kupitia kipindi kigumu kisoka msimu huu.

“Kuna kampeni dhidi yangu, lakini sitajiuzulu. Bado nipo hapa na mimi ndiye rais wa Real Madrid,” alisema Pérez mbele ya waandishi wa habari.

Perez pia alizungumzia uvumi uliosambaa kwenye mitandao ya kijamii ukidai kuwa anasumbuliwa na ugonjwa wa saratani, akisema taarifa hizo ni za kutungwa na hazina ukweli wowote.

“Watu wengine wanasema nina saratani. Hizi taarifa zimetengenezwa tu. Afya yangu iko imara,” alisisitiza.

Mkutano huo wa ghafla uliibua taharuki kubwa miongoni mwa mashabiki wa Real Madrid, huku wengi wakidhani huenda Pérez angejiuzulu kutokana na presha inayotokana na matokeo mabaya ya timu hiyo msimu huu. Real Madrid inaelekea kumaliza msimu bila taji kubwa kwa mwaka wa pili mfululizo, hali iliyoongeza lawama kwa uongozi wake.

Katika hotuba yake, Pérez alieleza kuwa bado ana nguvu na nia ya kuendelea kuiongoza klabu hiyo, huku akitangaza kuwa uchaguzi mpya wa uongozi wa Real Madrid utafanyika mapema kuliko ilivyotarajiwa na yeye mwenyewe atawania tena nafasi hiyo.

Florentino Pérez mwenye umri wa miaka 79 amekuwa mmoja wa marais waliofanikiwa zaidi katika historia ya Real Madrid, akiiongoza klabu hiyo kushinda mataji mengi ikiwemo UEFA Champions League mara kadhaa katika vipindi vyake viwili vya uongozi. 

More Stories

Barcelona yaendeleza kichapo Laliga ikimfunga Sevilla, Raphinha hashikiki.
Barcelona yaendeleza kichapo Laliga ikimfunga Sevilla, Raphinha hashikiki.
4h ago
READ MORE →
Mamelodi Sundowns yaibuka kidedea mbele ya Al Ahli
Mamelodi Sundowns yaibuka kidedea mbele ya Al Ahli
8h ago
READ MORE →
Arsenal yaduwazwa 3-0 na Brighton
Arsenal yaduwazwa 3-0 na Brighton
9h ago
READ MORE →
Nyota Stars waingia kambini tayari kwa mechi za kufuzu Afcon 2027
Nyota Stars waingia kambini tayari kwa mechi za kufuzu Afcon 2027
11h ago
READ MORE →
Simba kujichimbia Afrika Kusini kujiandaa na Kariakoo Derby
Simba kujichimbia Afrika Kusini kujiandaa na Kariakoo Derby
11h ago
READ MORE →
Madrid Derby: Atletico na Real kwenye vita ya majirani
Madrid Derby: Atletico na Real kwenye vita ya majirani
15h ago
READ MORE →
Hii hapa rekodi tamu ya Barker Ligi Kuu
Hii hapa rekodi tamu ya Barker Ligi Kuu
17h ago
READ MORE →
Sundowns kuchuana na Al Ahli katika vita ya Afrika na Asia
Sundowns kuchuana na Al Ahli katika vita ya Afrika na Asia
17h ago
READ MORE →
Ft: Yanga 1-0 St George, Yanga yapata ushindi mechi ya kirafiki.
Ft: Yanga 1-0 St George, Yanga yapata ushindi mechi ya kirafiki.
1d ago
READ MORE →
Dockers Derby yarudi baada ya miaka 14, Ulinzi wa London ukiimarishwa.
Dockers Derby yarudi baada ya miaka 14, Ulinzi wa London ukiimarishwa.
1d ago
READ MORE →