WPL : Simba Queens yaendeleza ubabe dhidi ya Yanga Princess

Joel JJ By Joel JJ β€’ 15th May 2026


WPL : Simba Queens yaendeleza ubabe dhidi ya Yanga Princess

Vinara wa Ligi Kuu ya Wanawake Tanzania, Simba Queens, wameendelea kuthibitisha ubora wao baada ya kuibuka na ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya watani zao Yanga Princess katika mchezo mkali uliopigwa kwenye uwanja wa Azam Complex.

Simba Queens walionyesha dhamira kubwa tangu dakika za mwanzo za mchezo huo, wakitawala sehemu kubwa ya kipindi cha kwanza na kufanikiwa kupata mabao mawili kupitia mshambuliaji wao hatari, Jentrix Shikangwa. Mabao hayo yaliwapa Simba faida muhimu mapema.

Kocha wa Simba Queens, Mussa Mgosi, alionekana kuingia na mkakati wa kumaliza mchezo mapema. Kikosi chake kilicheza kwa kasi na presha kubwa kipindi cha kwanza kabla ya kubadili mfumo katika kipindi cha pili kwa kucheza kwa tahadhari zaidi na kutumia mashambulizi ya kushtukiza.

Kwa upande wa Yanga Princess, kipindi cha kwanza kilikuwa kigumu huku wakionekana kuchelewa kuingia mchezoni. Hata hivyo, walirejea kwa nguvu kipindi cha pili na kupata bao la kufutia machozi kupitia kwa Riticcia Nabossa dakika ya 58. Bao hilo lilitokana na mpira wa adhabu uliopigwa na Precious Christopher baada ya Jeaninne Mukandayisenga kufanyiwa madhambi karibu na eneo la hatari.

Tukio hilo lilizua mjadala mkubwa kwani baadhi ya mashabiki waliamini Yanga Princess walistahili kupata penalti badala ya faulo ya nje, huku pia wakitaka mwamuzi kutoa adhabu kali zaidi kwa mchezaji wa Simba Queens aliyehusika.

Licha ya Yanga Princess kuongeza mashambulizi kipindi cha pili, juhudi zao hazikuzaa matunda mbele ya safu imara ya ulinzi ya Simba Queens.

Matokeo hayo yanaifanya Simba Queens kuendelea kuongoza msimamo wa ligi kwa alama 46, hatua inayoweka timu hiyo kwenye nafasi nzuri ya kutwaa ubingwa.

Kwa upande mwingine, Yanga Princess wamebaki nafasi ya pili wakiwa na alama 39, huku matumaini yao ya kuwania taji yakipungua baada ya kipigo hicho kutoka kwa watani zao.


  

More Stories

Azam Fc hiyooo fainali, yaichapa Yanga 3-2 nusu fainali
Azam Fc hiyooo fainali, yaichapa Yanga 3-2 nusu fainali
Today, READ MORE β†’
Azam Fc 3-2 Yanga, CRDB Cup
Azam Fc 3-2 Yanga, CRDB Cup
Today, READ MORE β†’
Ni Azam Fc vs Yanga, nani anakwenda fainali kombe la CRDB?
Ni Azam Fc vs Yanga, nani anakwenda fainali kombe la CRDB?
Today, READ MORE β†’
Liverpool kuongeza dau kumnasa Diomande
Liverpool kuongeza dau kumnasa Diomande
Today, READ MORE β†’
Prisons wamefufua matumaini kusalia ligi kuu
Prisons wamefufua matumaini kusalia ligi kuu
Today, READ MORE β†’
Tunisia yaaga kombe la Dunia kwa aibu, yapigwa 4-0 na Japan
Tunisia yaaga kombe la Dunia kwa aibu, yapigwa 4-0 na Japan
Today, READ MORE β†’
Ivory Coast yapoteza dhidi ya Ujerumani dakika za jioni
Ivory Coast yapoteza dhidi ya Ujerumani dakika za jioni
Today, READ MORE β†’
Real Madrid yakana kuwasiliana na Olise, wakala wake
Real Madrid yakana kuwasiliana na Olise, wakala wake
Yesterday, READ MORE β†’
Simba 4-0 Coastal Union, CRDB Cup
Simba 4-0 Coastal Union, CRDB Cup
Yesterday, READ MORE β†’
Simba yaifumua Coastal Union 4-0, yatinga fainali ya CRDB Bank Cup
Simba yaifumua Coastal Union 4-0, yatinga fainali ya CRDB Bank Cup
Yesterday, READ MORE β†’