Local,Normal News,Yanga, Simba

WPL : Simba Queens yaendeleza ubabe dhidi ya Yanga Princess

Joel JJ By Joel JJ
β€’
15 May 2026
WPL : Simba Queens yaendeleza ubabe dhidi ya Yanga Princess

Vinara wa Ligi Kuu ya Wanawake Tanzania, Simba Queens, wameendelea kuthibitisha ubora wao baada ya kuibuka na ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya watani zao Yanga Princess katika mchezo mkali uliopigwa kwenye uwanja wa Azam Complex.

Simba Queens walionyesha dhamira kubwa tangu dakika za mwanzo za mchezo huo, wakitawala sehemu kubwa ya kipindi cha kwanza na kufanikiwa kupata mabao mawili kupitia mshambuliaji wao hatari, Jentrix Shikangwa. Mabao hayo yaliwapa Simba faida muhimu mapema.

Kocha wa Simba Queens, Mussa Mgosi, alionekana kuingia na mkakati wa kumaliza mchezo mapema. Kikosi chake kilicheza kwa kasi na presha kubwa kipindi cha kwanza kabla ya kubadili mfumo katika kipindi cha pili kwa kucheza kwa tahadhari zaidi na kutumia mashambulizi ya kushtukiza.

Kwa upande wa Yanga Princess, kipindi cha kwanza kilikuwa kigumu huku wakionekana kuchelewa kuingia mchezoni. Hata hivyo, walirejea kwa nguvu kipindi cha pili na kupata bao la kufutia machozi kupitia kwa Riticcia Nabossa dakika ya 58. Bao hilo lilitokana na mpira wa adhabu uliopigwa na Precious Christopher baada ya Jeaninne Mukandayisenga kufanyiwa madhambi karibu na eneo la hatari.

Tukio hilo lilizua mjadala mkubwa kwani baadhi ya mashabiki waliamini Yanga Princess walistahili kupata penalti badala ya faulo ya nje, huku pia wakitaka mwamuzi kutoa adhabu kali zaidi kwa mchezaji wa Simba Queens aliyehusika.

Licha ya Yanga Princess kuongeza mashambulizi kipindi cha pili, juhudi zao hazikuzaa matunda mbele ya safu imara ya ulinzi ya Simba Queens.

Matokeo hayo yanaifanya Simba Queens kuendelea kuongoza msimamo wa ligi kwa alama 46, hatua inayoweka timu hiyo kwenye nafasi nzuri ya kutwaa ubingwa.

Kwa upande mwingine, Yanga Princess wamebaki nafasi ya pili wakiwa na alama 39, huku matumaini yao ya kuwania taji yakipungua baada ya kipigo hicho kutoka kwa watani zao.

More Stories

APR Fc yawaondosha aigles du congo kwenye caf champions league
APR Fc yawaondosha aigles du congo kwenye caf champions league
7h ago
READ MORE β†’
Azam Fc yaomboleza kifo cha mlinda lango U20
Azam Fc yaomboleza kifo cha mlinda lango U20
10h ago
READ MORE β†’
Hatuna presha kuikabili Yanga - Kocha Gaborone United
Hatuna presha kuikabili Yanga - Kocha Gaborone United
12h ago
READ MORE β†’
Manqoba aweka tahadhari mechi dhidi ya Gaborone United
Manqoba aweka tahadhari mechi dhidi ya Gaborone United
14h ago
READ MORE β†’
Rasmi: JoΓ£o Pedro Atwaa Tuzo Ya Mchezaji Bora Wa Mwezi Wa Agosti
Rasmi: JoΓ£o Pedro Atwaa Tuzo Ya Mchezaji Bora Wa Mwezi Wa Agosti
16h ago
READ MORE β†’
Simba inalenga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, nusu fainali ni lengo kubwa
Simba inalenga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, nusu fainali ni lengo kubwa
16h ago
READ MORE β†’
Libasse awapiga chini Max na Mwajanga, Kwenye tuzo za Mwezi.
Libasse awapiga chini Max na Mwajanga, Kwenye tuzo za Mwezi.
17h ago
READ MORE β†’
Fei Toto azipotezea Simba, Yanga
Fei Toto azipotezea Simba, Yanga
19h ago
READ MORE β†’
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 21, Septemba 11 2026
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 21, Septemba 11 2026
22h ago
READ MORE β†’
UEFA champions league: matokeo ya usiku
UEFA champions league: matokeo ya usiku
1d ago
READ MORE β†’