International,Transfer News,Real Madrid, Local

Mourinho akubaliana na masharti yote Real Madrid

Joel JJ By Joel JJ
16 May 2026
Mourinho akubaliana na masharti yote Real Madrid

Kocha Jose Mourinho anatajwa kuwa hatua za mwisho za kurejea kuinoa Real Madrid ambapo kulingana na Mwanahabari maarufu Fabrizio Romano, tayari amekubaliana na masharti yote ya mkataba wake mpya.

Fabrizio amebainisha kuwa mazungumzo kati ya Mourinho na rais wa Madrid, Florentino Pérez, yamekamilika kwa kiwango kikubwa huku kilichobaki kikiwa ni taratibu za mwisho kabla ya tangazo rasmi.

Mourinho ameweka masharti kadhaa muhimu kabla ya kurejea Santiago Bernabéu, ikiwemo uhuru mkubwa katika usajili wa wachezaji, maboresho ya kikosi pamoja na ushawishi mkubwa kwenye maamuzi ya kiufundi ndani ya klabu.

Kwa mujibu wa ripoti za hivi karibuni, uongozi wa Madrid umeonyesha utayari wa kukubaliana na matakwa hayo kutokana na presha ya kurejesha mafanikio ya haraka baada ya msimu wenye changamoto nyingi.

Vyanzo vya karibu na klabu vinaeleza kuwa Mourinho anaweza kutangazwa rasmi mara baada ya kumalizika kwa baadhi ya taratibu zinazomhusu na klabu yake ya sasa ya Benfica. Ripoti nyingine zinadai kuwa tayari kuna makubaliano ya muda wa mkataba pamoja na mipango ya usajili kwa ajili ya msimu ujao.

Mourinho aliwahi kuifundisha Real Madrid kati ya mwaka 2010 hadi 2013 ambapo aliisaidia kushinda mataji mbalimbali ikiwemo La Liga. Uongozi wa Madrid unaamini uzoefu wake mkubwa unaweza kurejesha nidhamu, ushindani na mafanikio ndani ya kikosi hicho.

More Stories

Barcelona yaendeleza kichapo Laliga ikimfunga Sevilla, Raphinha hashikiki.
Barcelona yaendeleza kichapo Laliga ikimfunga Sevilla, Raphinha hashikiki.
4h ago
READ MORE →
Mamelodi Sundowns yaibuka kidedea mbele ya Al Ahli
Mamelodi Sundowns yaibuka kidedea mbele ya Al Ahli
8h ago
READ MORE →
Arsenal yaduwazwa 3-0 na Brighton
Arsenal yaduwazwa 3-0 na Brighton
9h ago
READ MORE →
Nyota Stars waingia kambini tayari kwa mechi za kufuzu Afcon 2027
Nyota Stars waingia kambini tayari kwa mechi za kufuzu Afcon 2027
11h ago
READ MORE →
Simba kujichimbia Afrika Kusini kujiandaa na Kariakoo Derby
Simba kujichimbia Afrika Kusini kujiandaa na Kariakoo Derby
11h ago
READ MORE →
Madrid Derby: Atletico na Real kwenye vita ya majirani
Madrid Derby: Atletico na Real kwenye vita ya majirani
15h ago
READ MORE →
Hii hapa rekodi tamu ya Barker Ligi Kuu
Hii hapa rekodi tamu ya Barker Ligi Kuu
17h ago
READ MORE →
Sundowns kuchuana na Al Ahli katika vita ya Afrika na Asia
Sundowns kuchuana na Al Ahli katika vita ya Afrika na Asia
17h ago
READ MORE →
Ft: Yanga 1-0 St George, Yanga yapata ushindi mechi ya kirafiki.
Ft: Yanga 1-0 St George, Yanga yapata ushindi mechi ya kirafiki.
1d ago
READ MORE →
Dockers Derby yarudi baada ya miaka 14, Ulinzi wa London ukiimarishwa.
Dockers Derby yarudi baada ya miaka 14, Ulinzi wa London ukiimarishwa.
1d ago
READ MORE →