Mourinho akubaliana na masharti yote Real Madrid

Joel JJ By Joel JJ • 16th May 2026


Mourinho akubaliana na masharti yote Real Madrid

Kocha Jose Mourinho anatajwa kuwa hatua za mwisho za kurejea kuinoa Real Madrid ambapo kulingana na Mwanahabari maarufu Fabrizio Romano, tayari amekubaliana na masharti yote ya mkataba wake mpya.

Fabrizio amebainisha kuwa mazungumzo kati ya Mourinho na rais wa Madrid, Florentino Pérez, yamekamilika kwa kiwango kikubwa huku kilichobaki kikiwa ni taratibu za mwisho kabla ya tangazo rasmi.

Mourinho ameweka masharti kadhaa muhimu kabla ya kurejea Santiago Bernabéu, ikiwemo uhuru mkubwa katika usajili wa wachezaji, maboresho ya kikosi pamoja na ushawishi mkubwa kwenye maamuzi ya kiufundi ndani ya klabu.

Kwa mujibu wa ripoti za hivi karibuni, uongozi wa Madrid umeonyesha utayari wa kukubaliana na matakwa hayo kutokana na presha ya kurejesha mafanikio ya haraka baada ya msimu wenye changamoto nyingi.

Vyanzo vya karibu na klabu vinaeleza kuwa Mourinho anaweza kutangazwa rasmi mara baada ya kumalizika kwa baadhi ya taratibu zinazomhusu na klabu yake ya sasa ya Benfica. Ripoti nyingine zinadai kuwa tayari kuna makubaliano ya muda wa mkataba pamoja na mipango ya usajili kwa ajili ya msimu ujao.

Mourinho aliwahi kuifundisha Real Madrid kati ya mwaka 2010 hadi 2013 ambapo aliisaidia kushinda mataji mbalimbali ikiwemo La Liga. Uongozi wa Madrid unaamini uzoefu wake mkubwa unaweza kurejesha nidhamu, ushindani na mafanikio ndani ya kikosi hicho.


  

More Stories

Azam Fc hiyooo fainali, yaichapa Yanga 3-2 nusu fainali
Azam Fc hiyooo fainali, yaichapa Yanga 3-2 nusu fainali
Today, READ MORE →
Azam Fc 3-2 Yanga, CRDB Cup
Azam Fc 3-2 Yanga, CRDB Cup
Today, READ MORE →
Ni Azam Fc vs Yanga, nani anakwenda fainali kombe la CRDB?
Ni Azam Fc vs Yanga, nani anakwenda fainali kombe la CRDB?
Today, READ MORE →
Liverpool kuongeza dau kumnasa Diomande
Liverpool kuongeza dau kumnasa Diomande
Today, READ MORE →
Prisons wamefufua matumaini kusalia ligi kuu
Prisons wamefufua matumaini kusalia ligi kuu
Today, READ MORE →
Tunisia yaaga kombe la Dunia kwa aibu, yapigwa 4-0 na Japan
Tunisia yaaga kombe la Dunia kwa aibu, yapigwa 4-0 na Japan
Today, READ MORE →
Ivory Coast yapoteza dhidi ya Ujerumani dakika za jioni
Ivory Coast yapoteza dhidi ya Ujerumani dakika za jioni
Today, READ MORE →
Real Madrid yakana kuwasiliana na Olise, wakala wake
Real Madrid yakana kuwasiliana na Olise, wakala wake
Yesterday, READ MORE →
Simba 4-0 Coastal Union, CRDB Cup
Simba 4-0 Coastal Union, CRDB Cup
Yesterday, READ MORE →
Simba yaifumua Coastal Union 4-0, yatinga fainali ya CRDB Bank Cup
Simba yaifumua Coastal Union 4-0, yatinga fainali ya CRDB Bank Cup
Yesterday, READ MORE →