Kocha Simba apania kufuzu nusu fainali mbele ya TRA United

Joel JJ By Joel JJ โ€ข 16th May 2026


Kocha Simba apania kufuzu nusu fainali mbele ya TRA United

Kocha Mkuu wa Simba SC, Steve Barker, amesema anaamini kikosi chake kitakabiliana na mchezo mgumu dhidi ya TRA United katika hatua ya robo fainali ya Kombe la CRDB, huku akisisitiza kuwa maandalizi ya timu yake yamekamilika kwa kiwango kikubwa.

Simba SC itashuka dimbani kesho Jumapili, Mei 17, katika uwanja wa KMC Complex, kusaka tiketi ya kusonga mbele hatua ya nusu fainali ya mashindano hayo.

Akizungumza na waandishi wa habari leo, Barker alikiri ubora wa wapinzani wao TRA United, lakini akasisitiza kuwa kikosi chake kiko tayari kiakili na kimwili kwa changamoto hiyo.

โ€œTunakwenda kucheza dhidi ya timu nzuri na bora kwenye maeneo mengi, lakini sisi tumejiandaa kukabiliana na changamoto yoyote inayokuja mbele yetu,โ€ alisema Barker.

โ€œMorali ya wachezaji iko juu, tumefanya maandalizi mazuri kwa kuzingatia muda tuliopata. Tuko tayari kwenda kushinda mchezo huo,โ€ aliongeza.

Simba SC na TRA United zinakutana kwa mara ya tatu msimu huu, baada ya timu hizo kukutana mara mbili kwenye Ligi Kuu Tanzania Bara. Katika michezo hiyo, Simba ilishinda 3-0 katika mzunguko wa pili, huku mchezo wa kwanza ukimalizika kwa sare tasa ya 0-0 uliopigwa uwanja wa Sheikh Amri Abeid, Arusha.

Mchezo wa kesho unatarajiwa kuwa mkali na wenye ushindani mkubwa kutokana na kuwa mchezo wa maamuzi kusaka tiketi ya nusu fainali ya Kombe la CRDB.


  

More Stories

Azam Fc hiyooo fainali, yaichapa Yanga 3-2 nusu fainali
Azam Fc hiyooo fainali, yaichapa Yanga 3-2 nusu fainali
Today, READ MORE โ†’
Azam Fc 3-2 Yanga, CRDB Cup
Azam Fc 3-2 Yanga, CRDB Cup
Today, READ MORE โ†’
Ni Azam Fc vs Yanga, nani anakwenda fainali kombe la CRDB?
Ni Azam Fc vs Yanga, nani anakwenda fainali kombe la CRDB?
Today, READ MORE โ†’
Liverpool kuongeza dau kumnasa Diomande
Liverpool kuongeza dau kumnasa Diomande
Today, READ MORE โ†’
Prisons wamefufua matumaini kusalia ligi kuu
Prisons wamefufua matumaini kusalia ligi kuu
Today, READ MORE โ†’
Tunisia yaaga kombe la Dunia kwa aibu, yapigwa 4-0 na Japan
Tunisia yaaga kombe la Dunia kwa aibu, yapigwa 4-0 na Japan
Today, READ MORE โ†’
Ivory Coast yapoteza dhidi ya Ujerumani dakika za jioni
Ivory Coast yapoteza dhidi ya Ujerumani dakika za jioni
Today, READ MORE โ†’
Real Madrid yakana kuwasiliana na Olise, wakala wake
Real Madrid yakana kuwasiliana na Olise, wakala wake
Yesterday, READ MORE โ†’
Simba 4-0 Coastal Union, CRDB Cup
Simba 4-0 Coastal Union, CRDB Cup
Yesterday, READ MORE โ†’
Simba yaifumua Coastal Union 4-0, yatinga fainali ya CRDB Bank Cup
Simba yaifumua Coastal Union 4-0, yatinga fainali ya CRDB Bank Cup
Yesterday, READ MORE โ†’