Local,Normal News,Simba, TRA

Kocha Simba apania kufuzu nusu fainali mbele ya TRA United

Joel JJ By Joel JJ
16 May 2026
Kocha Simba apania kufuzu nusu fainali mbele ya TRA United

Kocha Mkuu wa Simba SC, Steve Barker, amesema anaamini kikosi chake kitakabiliana na mchezo mgumu dhidi ya TRA United katika hatua ya robo fainali ya Kombe la CRDB, huku akisisitiza kuwa maandalizi ya timu yake yamekamilika kwa kiwango kikubwa.

Simba SC itashuka dimbani kesho Jumapili, Mei 17, katika uwanja wa KMC Complex, kusaka tiketi ya kusonga mbele hatua ya nusu fainali ya mashindano hayo.

Akizungumza na waandishi wa habari leo, Barker alikiri ubora wa wapinzani wao TRA United, lakini akasisitiza kuwa kikosi chake kiko tayari kiakili na kimwili kwa changamoto hiyo.

“Tunakwenda kucheza dhidi ya timu nzuri na bora kwenye maeneo mengi, lakini sisi tumejiandaa kukabiliana na changamoto yoyote inayokuja mbele yetu,” alisema Barker.

“Morali ya wachezaji iko juu, tumefanya maandalizi mazuri kwa kuzingatia muda tuliopata. Tuko tayari kwenda kushinda mchezo huo,” aliongeza.

Simba SC na TRA United zinakutana kwa mara ya tatu msimu huu, baada ya timu hizo kukutana mara mbili kwenye Ligi Kuu Tanzania Bara. Katika michezo hiyo, Simba ilishinda 3-0 katika mzunguko wa pili, huku mchezo wa kwanza ukimalizika kwa sare tasa ya 0-0 uliopigwa uwanja wa Sheikh Amri Abeid, Arusha.

Mchezo wa kesho unatarajiwa kuwa mkali na wenye ushindani mkubwa kutokana na kuwa mchezo wa maamuzi kusaka tiketi ya nusu fainali ya Kombe la CRDB.

More Stories

Barcelona yaendeleza kichapo Laliga ikimfunga Sevilla, Raphinha hashikiki.
Barcelona yaendeleza kichapo Laliga ikimfunga Sevilla, Raphinha hashikiki.
5h ago
READ MORE →
Mamelodi Sundowns yaibuka kidedea mbele ya Al Ahli
Mamelodi Sundowns yaibuka kidedea mbele ya Al Ahli
10h ago
READ MORE →
Arsenal yaduwazwa 3-0 na Brighton
Arsenal yaduwazwa 3-0 na Brighton
10h ago
READ MORE →
Nyota Stars waingia kambini tayari kwa mechi za kufuzu Afcon 2027
Nyota Stars waingia kambini tayari kwa mechi za kufuzu Afcon 2027
12h ago
READ MORE →
Simba kujichimbia Afrika Kusini kujiandaa na Kariakoo Derby
Simba kujichimbia Afrika Kusini kujiandaa na Kariakoo Derby
13h ago
READ MORE →
Madrid Derby: Atletico na Real kwenye vita ya majirani
Madrid Derby: Atletico na Real kwenye vita ya majirani
16h ago
READ MORE →
Hii hapa rekodi tamu ya Barker Ligi Kuu
Hii hapa rekodi tamu ya Barker Ligi Kuu
18h ago
READ MORE →
Sundowns kuchuana na Al Ahli katika vita ya Afrika na Asia
Sundowns kuchuana na Al Ahli katika vita ya Afrika na Asia
19h ago
READ MORE →
Ft: Yanga 1-0 St George, Yanga yapata ushindi mechi ya kirafiki.
Ft: Yanga 1-0 St George, Yanga yapata ushindi mechi ya kirafiki.
1d ago
READ MORE →
Dockers Derby yarudi baada ya miaka 14, Ulinzi wa London ukiimarishwa.
Dockers Derby yarudi baada ya miaka 14, Ulinzi wa London ukiimarishwa.
1d ago
READ MORE →