International,Normal News,Barcelona, Local

Barcelona wameweka rekodi ya kibabe nyumbani La Liga

Joel JJ By Joel JJ
18 May 2026
Barcelona wameweka rekodi ya kibabe nyumbani La Liga

Klabu ya FC Barcelona imeandika historia katika Ligi Kuu ya Hispania (La Liga) msimu huu 2025/26 baada ya kumaliza msimu wa mechi za nyumbani bila kupoteza, hatua iliyoweka rekodi mpya ya kutokufungwa katika dimba lao la nyumbani.

Msimu huu, Barcelona chini ya kocha Hansi Flick wamefanikiwa kushinda mechi zote 19 za nyumbani bila kupoteza, hali iliyowafanya kuwa timu yenye uimara mkubwa zaidi nyumbani barani Ulaya.

Mfululizo huo wa matokeo umejengwa juu ya nidhamu ya kiufundi, uimara wa safu ya ulinzi pamoja na uwezo mkubwa wa ushambuliaji uliosheheni wachezaji kama Lamine Yamal, Robert Lewandowski, Raphinha, Pedri, Marcus Rashford, Ferran na Fermín López ambao wamekuwa nguzo muhimu katika mafanikio ya timu hiyo.

Barcelona pia wameonyesha ubora mkubwa wa kiufundi katika mechi zao za nyumbani, wakidhibiti michezo mingi kwa umiliki wa mpira na kutumia vyema nafasi wanazopata mbele ya lango la wapinzani wao.

Rekodi hii inatajwa kama mojawapo ya mafanikio makubwa ya klabu hiyo katika miaka ya hivi karibuni, huku ikiwapa nafasi ya kuendelea kuimarisha hadhi yao kama moja ya timu bora za soka barani Ulaya.

Mabingwa hao wa La Liga kwa misimu miwili mfululizo, wametangaza kumuongeza mkataba kocha Hansi Flick ambapo ataendelea kusalia Camp Nou hadi mwaka 2028.

More Stories

Barcelona yaendeleza kichapo Laliga ikimfunga Sevilla, Raphinha hashikiki.
Barcelona yaendeleza kichapo Laliga ikimfunga Sevilla, Raphinha hashikiki.
6h ago
READ MORE →
Mamelodi Sundowns yaibuka kidedea mbele ya Al Ahli
Mamelodi Sundowns yaibuka kidedea mbele ya Al Ahli
11h ago
READ MORE →
Arsenal yaduwazwa 3-0 na Brighton
Arsenal yaduwazwa 3-0 na Brighton
11h ago
READ MORE →
Nyota Stars waingia kambini tayari kwa mechi za kufuzu Afcon 2027
Nyota Stars waingia kambini tayari kwa mechi za kufuzu Afcon 2027
13h ago
READ MORE →
Simba kujichimbia Afrika Kusini kujiandaa na Kariakoo Derby
Simba kujichimbia Afrika Kusini kujiandaa na Kariakoo Derby
14h ago
READ MORE →
Madrid Derby: Atletico na Real kwenye vita ya majirani
Madrid Derby: Atletico na Real kwenye vita ya majirani
17h ago
READ MORE →
Hii hapa rekodi tamu ya Barker Ligi Kuu
Hii hapa rekodi tamu ya Barker Ligi Kuu
19h ago
READ MORE →
Sundowns kuchuana na Al Ahli katika vita ya Afrika na Asia
Sundowns kuchuana na Al Ahli katika vita ya Afrika na Asia
20h ago
READ MORE →
Ft: Yanga 1-0 St George, Yanga yapata ushindi mechi ya kirafiki.
Ft: Yanga 1-0 St George, Yanga yapata ushindi mechi ya kirafiki.
1d ago
READ MORE →
Dockers Derby yarudi baada ya miaka 14, Ulinzi wa London ukiimarishwa.
Dockers Derby yarudi baada ya miaka 14, Ulinzi wa London ukiimarishwa.
1d ago
READ MORE →