International,Normal News,Southampton

Southampton yapatikana na hatia ya kupeleleza wapinzani

Joel JJ By Joel JJ
β€’
20 May 2026
Southampton yapatikana na hatia ya kupeleleza wapinzani

Klabu ya Southampton FC imejikuta kwenye wakati mgumu baada ya kupewa adhabu kali na English Football League (EFL) kufuatia tuhuma za upelelezi dhidi ya wapinzani wao wa Championship play-offs.

Kwa mujibu wa taarifa rasmi ya EFL, Southampton imeondolewa kwenye fainali ya Championship play-offs na pia imepewa adhabu ya kupokwa pointi nne zitakazotumika msimu wa 2026/27.

Kisa kilichoibua sakata hilo

Sakata hilo limepewa jina la β€œSpygate 2.0” baada ya madai kwamba baadhi ya wafanyakazi wa Southampton walinaswa wakirekodi mazoezi ya Middlesbrough FC kabla ya mchezo wa nusu fainali ya play-offs.

Ripoti zinaeleza kuwa uchunguzi wa EFL ulibaini Southampton walikiuka kanuni ya 127 ya ligi hiyo inayokataza timu kufuatilia au kurekodi mazoezi ya mpinzani ndani ya saa 72 kabla ya mchezo.

Mbali na Middlesbrough, uchunguzi pia ulidai kuwa Southampton walihusika kufuatilia mazoezi ya Oxford United na Ipswich Town katika baadhi ya mechi za msimu huu.

Adhabu yenye maumivu makubwa

Adhabu hiyo imekuwa pigo kubwa kwa Southampton kwa sababu ilikuwa imefuzu kucheza fainali ya kuwania kupanda Ligi Kuu England (Premier League), mchezo unaotajwa kuwa miongoni mwa mechi zenye thamani kubwa zaidi kifedha duniani.

Taarifa mbalimbali zinaonyesha timu inayopanda Premier League inaweza kupata zaidi ya pauni milioni 200 kupitia haki za matangazo, udhamini na mapato mengine.

Kutokana na adhabu hiyo, Middlesbrough sasa imerejeshwa kwenye fainali na itacheza dhidi ya Hull City katika pambano la kuwania kupanda daraja.

Southampton yapanga kukata rufaa

Uongozi wa Southampton tayari umetangaza kuwa utaendelea kushirikiana na EFL huku ukipanga kukata rufaa dhidi ya uamuzi huo.

Wachambuzi wa soka nchini England wanaamini sakata hili linaweza kuwa moja ya maamuzi makubwa zaidi kuwahi kutolewa katika historia ya Championship, hasa baada ya EFL kuamua kuchukua msimamo mkali tofauti na tukio la mwaka 2019 lililohusisha Leeds United ambapo timu hiyo iliishia kutozwa faini pekee.

More Stories

Barcelona yaendeleza kichapo Laliga ikimfunga Sevilla, Raphinha hashikiki.
Barcelona yaendeleza kichapo Laliga ikimfunga Sevilla, Raphinha hashikiki.
4h ago
READ MORE β†’
Mamelodi Sundowns yaibuka kidedea mbele ya Al Ahli
Mamelodi Sundowns yaibuka kidedea mbele ya Al Ahli
8h ago
READ MORE β†’
Arsenal yaduwazwa 3-0 na Brighton
Arsenal yaduwazwa 3-0 na Brighton
9h ago
READ MORE β†’
Nyota Stars waingia kambini tayari kwa mechi za kufuzu Afcon 2027
Nyota Stars waingia kambini tayari kwa mechi za kufuzu Afcon 2027
11h ago
READ MORE β†’
Simba kujichimbia Afrika Kusini kujiandaa na Kariakoo Derby
Simba kujichimbia Afrika Kusini kujiandaa na Kariakoo Derby
11h ago
READ MORE β†’
Madrid Derby: Atletico na Real kwenye vita ya majirani
Madrid Derby: Atletico na Real kwenye vita ya majirani
15h ago
READ MORE β†’
Hii hapa rekodi tamu ya Barker Ligi Kuu
Hii hapa rekodi tamu ya Barker Ligi Kuu
17h ago
READ MORE β†’
Sundowns kuchuana na Al Ahli katika vita ya Afrika na Asia
Sundowns kuchuana na Al Ahli katika vita ya Afrika na Asia
17h ago
READ MORE β†’
Ft: Yanga 1-0 St George, Yanga yapata ushindi mechi ya kirafiki.
Ft: Yanga 1-0 St George, Yanga yapata ushindi mechi ya kirafiki.
1d ago
READ MORE β†’
Dockers Derby yarudi baada ya miaka 14, Ulinzi wa London ukiimarishwa.
Dockers Derby yarudi baada ya miaka 14, Ulinzi wa London ukiimarishwa.
1d ago
READ MORE β†’