Local,Transfer News,Singida

Rupia na Singida BS ndio basi tena

Joel JJ By Joel JJ
β€’
20 May 2026
Rupia na Singida BS ndio basi tena

Baada ya sintofahamu ya wiki kadhaa, inaelezwa klabu ya Singida Black Stars na mshambuliaji wake wa kimataifa kutoka Kenya, Elvis Rupia, wamefikia makubaliano ya pande mbili kusitisha mkataba.

Hatua hii inakuja ikiwa ni mwendelezo wa taarifa zilizokuwa zikisambaa awali, zikieleza kuwa Rupia alijiondoa kambini kutokana na madai mbalimbali kwa uongozi wa Singida BS.

Awali, Rupia aliondoka katika mazingira yaliyozua maswali kwa mashabiki wa Singida BS, akiwa hajaonekana kwenye kikosi cha timu hiyo kwa wiki kadhaa.

Inadaiwa kuwa chanzo kikuu cha sintofahamu hiyo kilikuwa ni madai ya stahiki mbalimbali kulingana na makubaliano ya kimkataba baina yake na Singida BS.

Rupia ameichezea Singida Black Stars kwa takribani misimu mitatu, akiwa miongoni mwa washambuliaji waliotoa mchango mkubwa katika safu ya ushambuliaji ya timu hiyo. Sasa yuko huru kujiunga na klabu nyingine katika dirisha lijalo la usajili litakalofunguliwa baada ya msimu huu kufika tamati.

More Stories

APR Fc yawaondosha aigles du congo kwenye caf champions league
APR Fc yawaondosha aigles du congo kwenye caf champions league
2h ago
READ MORE β†’
Azam Fc yaomboleza kifo cha mlinda lango U20
Azam Fc yaomboleza kifo cha mlinda lango U20
5h ago
READ MORE β†’
Hatuna presha kuikabili Yanga - Kocha Gaborone United
Hatuna presha kuikabili Yanga - Kocha Gaborone United
7h ago
READ MORE β†’
Manqoba aweka tahadhari mechi dhidi ya Gaborone United
Manqoba aweka tahadhari mechi dhidi ya Gaborone United
9h ago
READ MORE β†’
Rasmi: JoΓ£o Pedro Atwaa Tuzo Ya Mchezaji Bora Wa Mwezi Wa Agosti
Rasmi: JoΓ£o Pedro Atwaa Tuzo Ya Mchezaji Bora Wa Mwezi Wa Agosti
11h ago
READ MORE β†’
Simba inalenga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, nusu fainali ni lengo kubwa
Simba inalenga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, nusu fainali ni lengo kubwa
11h ago
READ MORE β†’
Libasse awapiga chini Max na Mwajanga, Kwenye tuzo za Mwezi.
Libasse awapiga chini Max na Mwajanga, Kwenye tuzo za Mwezi.
12h ago
READ MORE β†’
Fei Toto azipotezea Simba, Yanga
Fei Toto azipotezea Simba, Yanga
14h ago
READ MORE β†’
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 21, Septemba 11 2026
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 21, Septemba 11 2026
17h ago
READ MORE β†’
UEFA champions league: matokeo ya usiku
UEFA champions league: matokeo ya usiku
1d ago
READ MORE β†’