Zamalek mabingwa Misri, Al Ahly majanga

Joel JJ By Joel JJ β€’ 21st May 2026


Zamalek mabingwa Misri, Al Ahly majanga

Klabu ya Zamalek SC imetwaa ubingwa wa Ligi Kuu ya Misri kwa msimu wa 2025/26 baada ya kuibuka na ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Ceramica Cleopatra FC katika mchezo wa mwisho wa msimu uliochezwa jijini Cairo.

Ushindi huo umeifanya Zamalek kufikisha pointi 56 na kutwaa taji lao la 15 katika historia ya ligi hiyo, baada ya ushindani mkali uliodumu hadi dakika za mwisho za msimu.

Katika msimamo wa mwisho, Pyramids FC walimaliza nafasi ya pili wakiwa na pointi 54 baada ya kushinda mchezo wao wa mwisho, huku Al Ahly wakimaliza nafasi ya tatu licha ya kuifunga Al Masry mabao 2-0.

Matokeo hayo yanamaanisha kuwa Zamalek na Pyramids FC wataiwakilisha Misri kwenye mashindano ya CAF Champions League msimu ujao, huku Al Ahly wakilazimika kushiriki Kombe la Shirikisho Afrika (CAF Confederation Cup).

Ni mara ya kwanza tangu mwaka 2003 kwa Al Ahly kukosa nafasi ya kushiriki CAF Champions League, jambo ambalo limezua mjadala mkubwa kutokana na historia kubwa ya klabu hiyo barani Afrika ambapo imewahi kutwaa taji hilo mara 12.

Msimu huu wa ligi kuu ya Misri ulikuwa na ushindani mkubwa kati ya timu hizo tatu hadi mzunguko wa mwisho, huku Zamalek wakifanikiwa kutumia vyema nafasi yao ya mwisho na kutwaa ubingwa mbele ya mahasimu wao wakubwa.


  

More Stories

Azam Fc hiyooo fainali, yaichapa Yanga 3-2 nusu fainali
Azam Fc hiyooo fainali, yaichapa Yanga 3-2 nusu fainali
Today, READ MORE β†’
Azam Fc 3-2 Yanga, CRDB Cup
Azam Fc 3-2 Yanga, CRDB Cup
Today, READ MORE β†’
Ni Azam Fc vs Yanga, nani anakwenda fainali kombe la CRDB?
Ni Azam Fc vs Yanga, nani anakwenda fainali kombe la CRDB?
Today, READ MORE β†’
Liverpool kuongeza dau kumnasa Diomande
Liverpool kuongeza dau kumnasa Diomande
Today, READ MORE β†’
Prisons wamefufua matumaini kusalia ligi kuu
Prisons wamefufua matumaini kusalia ligi kuu
Today, READ MORE β†’
Tunisia yaaga kombe la Dunia kwa aibu, yapigwa 4-0 na Japan
Tunisia yaaga kombe la Dunia kwa aibu, yapigwa 4-0 na Japan
Today, READ MORE β†’
Ivory Coast yapoteza dhidi ya Ujerumani dakika za jioni
Ivory Coast yapoteza dhidi ya Ujerumani dakika za jioni
Today, READ MORE β†’
Real Madrid yakana kuwasiliana na Olise, wakala wake
Real Madrid yakana kuwasiliana na Olise, wakala wake
Yesterday, READ MORE β†’
Simba 4-0 Coastal Union, CRDB Cup
Simba 4-0 Coastal Union, CRDB Cup
Yesterday, READ MORE β†’
Simba yaifumua Coastal Union 4-0, yatinga fainali ya CRDB Bank Cup
Simba yaifumua Coastal Union 4-0, yatinga fainali ya CRDB Bank Cup
Yesterday, READ MORE β†’