International,Normal News,Zamalek, Pyramids, Al Ahly, Local

Zamalek mabingwa Misri, Al Ahly majanga

Joel JJ By Joel JJ
β€’
21 May 2026
Zamalek mabingwa Misri, Al Ahly majanga

Klabu ya Zamalek SC imetwaa ubingwa wa Ligi Kuu ya Misri kwa msimu wa 2025/26 baada ya kuibuka na ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Ceramica Cleopatra FC katika mchezo wa mwisho wa msimu uliochezwa jijini Cairo.

Ushindi huo umeifanya Zamalek kufikisha pointi 56 na kutwaa taji lao la 15 katika historia ya ligi hiyo, baada ya ushindani mkali uliodumu hadi dakika za mwisho za msimu.

Katika msimamo wa mwisho, Pyramids FC walimaliza nafasi ya pili wakiwa na pointi 54 baada ya kushinda mchezo wao wa mwisho, huku Al Ahly wakimaliza nafasi ya tatu licha ya kuifunga Al Masry mabao 2-0.

Matokeo hayo yanamaanisha kuwa Zamalek na Pyramids FC wataiwakilisha Misri kwenye mashindano ya CAF Champions League msimu ujao, huku Al Ahly wakilazimika kushiriki Kombe la Shirikisho Afrika (CAF Confederation Cup).

Ni mara ya kwanza tangu mwaka 2003 kwa Al Ahly kukosa nafasi ya kushiriki CAF Champions League, jambo ambalo limezua mjadala mkubwa kutokana na historia kubwa ya klabu hiyo barani Afrika ambapo imewahi kutwaa taji hilo mara 12.

Msimu huu wa ligi kuu ya Misri ulikuwa na ushindani mkubwa kati ya timu hizo tatu hadi mzunguko wa mwisho, huku Zamalek wakifanikiwa kutumia vyema nafasi yao ya mwisho na kutwaa ubingwa mbele ya mahasimu wao wakubwa.

More Stories

APR Fc yawaondosha aigles du congo kwenye caf champions league
APR Fc yawaondosha aigles du congo kwenye caf champions league
1h ago
READ MORE β†’
Azam Fc yaomboleza kifo cha mlinda lango U20
Azam Fc yaomboleza kifo cha mlinda lango U20
4h ago
READ MORE β†’
Hatuna presha kuikabili Yanga - Kocha Gaborone United
Hatuna presha kuikabili Yanga - Kocha Gaborone United
6h ago
READ MORE β†’
Manqoba aweka tahadhari mechi dhidi ya Gaborone United
Manqoba aweka tahadhari mechi dhidi ya Gaborone United
8h ago
READ MORE β†’
Rasmi: JoΓ£o Pedro Atwaa Tuzo Ya Mchezaji Bora Wa Mwezi Wa Agosti
Rasmi: JoΓ£o Pedro Atwaa Tuzo Ya Mchezaji Bora Wa Mwezi Wa Agosti
10h ago
READ MORE β†’
Simba inalenga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, nusu fainali ni lengo kubwa
Simba inalenga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, nusu fainali ni lengo kubwa
11h ago
READ MORE β†’
Libasse awapiga chini Max na Mwajanga, Kwenye tuzo za Mwezi.
Libasse awapiga chini Max na Mwajanga, Kwenye tuzo za Mwezi.
11h ago
READ MORE β†’
Fei Toto azipotezea Simba, Yanga
Fei Toto azipotezea Simba, Yanga
13h ago
READ MORE β†’
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 21, Septemba 11 2026
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 21, Septemba 11 2026
16h ago
READ MORE β†’
UEFA champions league: matokeo ya usiku
UEFA champions league: matokeo ya usiku
1d ago
READ MORE β†’