Local,Transfer News,Simba

Chama mbioni kuongeza mkataba mpya Simba

Joel JJ By Joel JJ
β€’
21 May 2026
Chama mbioni kuongeza mkataba mpya Simba

Kiungo mshambuliaji Clatous Chama anatarajiwa kuendelea kuitumikia Simba SC baada ya kuingia kwenye hatua za mwisho za mazungumzo ya kuongeza mkataba mpya ndani ya kikosi hicho cha Wekundu wa Msimbazi, imefahamika.

Chama, ambaye alirejea Simba akitokea Singida Big Stars SC, alisaini awali mkataba wa mwaka mmoja, lakini sasa taarifa zinaeleza kuwa mazungumzo ya kuongeza kandarasi ya ziada ya mwaka mmoja yamekamilika kwa mafanikio.

Kwa mujibu wa vyanzo kutoka ndani ya uongozi wa Simba, mkataba mpya wa kiungo huyo sasa unatarajiwa kumfanya abaki klabuni hapo hadi mwaka 2028, hatua inayoonekana kuwa sehemu ya mkakati wa klabu kuimarisha kikosi chake cha ushindani.

Uongozi wa Simba umechukua hatua ya mapema kuhakikisha nyota huyo anasaini mkataba mpya kabla ya msimu wa mashindano kufikia tamati, ili kuondoa uwezekano wa vilabu vingine kuingia kwenye vita ya kumsajili.

Tangu aliporejea Msimbazi kupitia dirisha dogo, Chama ameendelea kuwa mchezaji muhimu katika mfumo wa timu, akichangia mabao nane katika mashindano yote na kuonyesha kiwango kinachovutia mashabiki na wadau wa soka nchini.

Mbali na mchango wake wa mabao, kiungo huyo kutoka Zambia pia ameweka rekodi ya kutwaa tuzo ya mchezaji bora wa mchezo katika mechi nne mfululizo, hali inayoonyesha ubora wake na umuhimu wake ndani ya kikosi cha Simba.

More Stories

Barcelona yaendeleza kichapo Laliga ikimfunga Sevilla, Raphinha hashikiki.
Barcelona yaendeleza kichapo Laliga ikimfunga Sevilla, Raphinha hashikiki.
2h ago
READ MORE β†’
Mamelodi Sundowns yaibuka kidedea mbele ya Al Ahli
Mamelodi Sundowns yaibuka kidedea mbele ya Al Ahli
6h ago
READ MORE β†’
Arsenal yaduwazwa 3-0 na Brighton
Arsenal yaduwazwa 3-0 na Brighton
7h ago
READ MORE β†’
Nyota Stars waingia kambini tayari kwa mechi za kufuzu Afcon 2027
Nyota Stars waingia kambini tayari kwa mechi za kufuzu Afcon 2027
9h ago
READ MORE β†’
Simba kujichimbia Afrika Kusini kujiandaa na Kariakoo Derby
Simba kujichimbia Afrika Kusini kujiandaa na Kariakoo Derby
9h ago
READ MORE β†’
Madrid Derby: Atletico na Real kwenye vita ya majirani
Madrid Derby: Atletico na Real kwenye vita ya majirani
13h ago
READ MORE β†’
Hii hapa rekodi tamu ya Barker Ligi Kuu
Hii hapa rekodi tamu ya Barker Ligi Kuu
15h ago
READ MORE β†’
Sundowns kuchuana na Al Ahli katika vita ya Afrika na Asia
Sundowns kuchuana na Al Ahli katika vita ya Afrika na Asia
15h ago
READ MORE β†’
Ft: Yanga 1-0 St George, Yanga yapata ushindi mechi ya kirafiki.
Ft: Yanga 1-0 St George, Yanga yapata ushindi mechi ya kirafiki.
1d ago
READ MORE β†’
Dockers Derby yarudi baada ya miaka 14, Ulinzi wa London ukiimarishwa.
Dockers Derby yarudi baada ya miaka 14, Ulinzi wa London ukiimarishwa.
1d ago
READ MORE β†’