Shirikisho la Soka la Senegal limetangaza rasmi kikosi cha wachezaji 26 kitakachoshiriki Kombe la Dunia 2026, kikiongozwa na nahodha na nyota wake wa ushambuliaji Sadio Mané.
Kikosi hicho kimetangazwa na kocha mkuu Pape Thiaw, kikiwa na mchanganyiko wa wachezaji wenye uzoefu mkubwa pamoja na vipaji chipukizi vinavyocheza katika ligi mbalimbali barani Ulaya na Asia.





