Yanga, Azam Fc viwanjani ligi kuu leo May 22

Joel JJ By Joel JJ β€’ 22nd May 2026


Yanga, Azam Fc viwanjani ligi kuu leo May 22

Ligi Kuu ya NBC inaendelea leo ambapo mechi mbili za kuhitimisha raundi ya 24 zitapigwa jijini Dar es salaam.

Mabingwa watetezi wa ligi hiyo Yanga watakuwa dimba la KMC Complex kuikabili Singida BS katika mchezo utakaopigwa saa 10 jioni.

Baada ya watani zao Simba kuwaondoa kileleni mwa msimamo wa ligi jana baada ya ushindi wa mabao 2-1 dhidi yq Coastal Union, ni wazi Yanga leo itahitaji ushindi ili kurejea tena juu ya msimamo.

Hata hivyo haitakuwa rahisi mbele ya Singida BS ambayo baada ya kutupwa nje ya michuano ya kombe la CRDB, matumaini yao kushiriki michuano ya CAF msimu ujao ni kumaliza angalau nafasi ya nne.

Yanga iliibuka na ushindi wa mabao 3-0 kwenye mchezo wa duru ya kwanza uliopigwa Singida hivyo leo Wananchi watataka kuendeleza ubabe wao dhidi ya walima alizeti hao.

Mchezo mwingine utakaopigwa leo ni kati ya Azam Fc dhidi ya Tanzania Prisons utakaopigwa saa 12:30 jioni uwanja wa Azam Complex.

Prisons wako eneo jekundu la kushuka daraja wanahoitaji kupata alama kwenye kila mchezo lakini habari mbaya kwao ni kuwa wanakutana na Azam Fc ambao bado imeweka presha katika mbio za ubingwa.


  

More Stories

Azam Fc hiyooo fainali, yaichapa Yanga 3-2 nusu fainali
Azam Fc hiyooo fainali, yaichapa Yanga 3-2 nusu fainali
Today, READ MORE β†’
Azam Fc 3-2 Yanga, CRDB Cup
Azam Fc 3-2 Yanga, CRDB Cup
Today, READ MORE β†’
Ni Azam Fc vs Yanga, nani anakwenda fainali kombe la CRDB?
Ni Azam Fc vs Yanga, nani anakwenda fainali kombe la CRDB?
Today, READ MORE β†’
Liverpool kuongeza dau kumnasa Diomande
Liverpool kuongeza dau kumnasa Diomande
Today, READ MORE β†’
Prisons wamefufua matumaini kusalia ligi kuu
Prisons wamefufua matumaini kusalia ligi kuu
Today, READ MORE β†’
Tunisia yaaga kombe la Dunia kwa aibu, yapigwa 4-0 na Japan
Tunisia yaaga kombe la Dunia kwa aibu, yapigwa 4-0 na Japan
Today, READ MORE β†’
Ivory Coast yapoteza dhidi ya Ujerumani dakika za jioni
Ivory Coast yapoteza dhidi ya Ujerumani dakika za jioni
Today, READ MORE β†’
Real Madrid yakana kuwasiliana na Olise, wakala wake
Real Madrid yakana kuwasiliana na Olise, wakala wake
Yesterday, READ MORE β†’
Simba 4-0 Coastal Union, CRDB Cup
Simba 4-0 Coastal Union, CRDB Cup
Yesterday, READ MORE β†’
Simba yaifumua Coastal Union 4-0, yatinga fainali ya CRDB Bank Cup
Simba yaifumua Coastal Union 4-0, yatinga fainali ya CRDB Bank Cup
Yesterday, READ MORE β†’