Local,Normal News,Ligi Kuu, Simba, Dodoma Jiji

Simba yakiri ugumu wa Dodoma Jiji, yapania ushindi KMC Complex

Joel JJ By Joel JJ
β€’
23 May 2026
Simba yakiri ugumu wa Dodoma Jiji, yapania ushindi KMC Complex

Kocha Msaidizi wa Simba SC, Suleiman Matola, amesema mchezo wa Ligi Kuu Tanzania Bara dhidi ya Dodoma Jiji FC utakaopigwa kesho Jumapili katika uwanja wa KMC Complex hautakuwa mwepesi, akisisitiza kuwa wapinzani wao ni timu yenye ubora na ushindani mkubwa.

Akizungumza na wanahabari kuelekea mchezo huo, Matola amesema wanakumbuka ugumu walioupata mara ya mwisho walipokutana na Dodoma Jiji mkoani Dodoma, ambapo mchezo huo uliishia kwa suluhu ya bila kufungana.

Hata hivyo, amesisitiza kuwa Simba imejipanga vyema kuhakikisha inapata alama zote tatu muhimu zitakazowasaidia kurejea kileleni mwa msimamo wa ligi.

“Haitakuwa mechi rahisi ukiangalia matokeo ya mchezo uliopita, Dodoma Jiji walitupa wakati mgumu,” alisema Matola.

“Lakini pamoja na ugumu na ubora wao, tumejipanga kuhakikisha tunapata pointi tatu katika mchezo huo.”

Wakati huo huo, kikosi cha Simba kilirejea jijini Dar es Salaam jana kikitokea mkoani Tanga, ambako kiliibuka na ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya Coastal Union, matokeo ambayo yameongeza morali ndani ya kikosi hicho kabla ya mchezo huu muhimu wa ligi.

More Stories

Mamelodi Sundowns yaibuka kidedea mbele ya Al Ahli
Mamelodi Sundowns yaibuka kidedea mbele ya Al Ahli
2h ago
READ MORE β†’
Arsenal yaduwazwa 3-0 na Brighton
Arsenal yaduwazwa 3-0 na Brighton
3h ago
READ MORE β†’
Nyota Stars waingia kambini tayari kwa mechi za kufuzu Afcon 2027
Nyota Stars waingia kambini tayari kwa mechi za kufuzu Afcon 2027
5h ago
READ MORE β†’
Simba kujichimbia Afrika Kusini kujiandaa na Kariakoo Derby
Simba kujichimbia Afrika Kusini kujiandaa na Kariakoo Derby
5h ago
READ MORE β†’
Madrid Derby: Atletico na Real kwenye vita ya majirani
Madrid Derby: Atletico na Real kwenye vita ya majirani
9h ago
READ MORE β†’
Hii hapa rekodi tamu ya Barker Ligi Kuu
Hii hapa rekodi tamu ya Barker Ligi Kuu
11h ago
READ MORE β†’
Sundowns kuchuana na Al Ahli katika vita ya Afrika na Asia
Sundowns kuchuana na Al Ahli katika vita ya Afrika na Asia
11h ago
READ MORE β†’
Ft: Yanga 1-0 St George, Yanga yapata ushindi mechi ya kirafiki.
Ft: Yanga 1-0 St George, Yanga yapata ushindi mechi ya kirafiki.
1d ago
READ MORE β†’
Dockers Derby yarudi baada ya miaka 14, Ulinzi wa London ukiimarishwa.
Dockers Derby yarudi baada ya miaka 14, Ulinzi wa London ukiimarishwa.
1d ago
READ MORE β†’
Kocha Dimitar Pantev ateuliwa kuwa kocha mpya wa Richard Bay.
Kocha Dimitar Pantev ateuliwa kuwa kocha mpya wa Richard Bay.
1d ago
READ MORE β†’