Local,Normal News,Singida BS, Yanga

Metacha aomba radhi baada ya tukio la kugomea mabadiliko

Joel JJ By Joel JJ
24 May 2026
Metacha aomba radhi baada ya tukio la kugomea mabadiliko

Golikipa wa Singida Black Stars, Metacha Mnata ameomba radhi kufuatia tukio la kugomea kufanyiwa mabadiliko katika mchezo wa Ligi Kuu Tanzania Bara dhidi ya Young Africans SC uliochezwa uwanja wa KMC Complex juzi Singida BS wakikubali kipigo cha mabao 3-0.

Mnata alionekana kutokuwa tayari kutoka uwanjani muda mfupi baada ya kuruhusu bao kupitia mpira wa adhabu, kabla ya baadaye kukubali nafasi yake kuchukuliwa na golikipa mwingine wa timu hiyo, Abasogie Amos.

Kupitia ujumbe wake, Mnata amesema tukio hilo lilitokana na presha ya mchezo na hisia za ushindani, huku akisisitiza kuwa hakuwa na nia ya kuonyesha utovu wa nidhamu au kupuuza maamuzi ya benchi la ufundi.

“Naomba radhi kwa Mashabiki, Benchi la Ufundi, Viongozi na wapenzi wote wa Singida BS kutokana na sintofahamu iliyotokea kwenye mchezo wetu dhidi ya Young Africans SC.”

“Kilichotokea kilikuwa ni matokeo ya hisia za mchezo na presha ya ushindani, lakini haikuwa dhamira yangu kuonyesha utovu wa nidhamu wala kudharau maamuzi ya Benchi la Ufundi.”

“Ninaiheshimu timu yangu, kocha wangu na maamuzi yote yanayofanywa kwa maslahi ya klabu. Nimejifunza kutokana na tukio lile na nawaahidi nitaendelea kupambana kwa ajili ya timu kwa nidhamu, kujituma na mshikamano mkubwa zaidi na wenzangu,” alisema Metacha.

Baada ya kuomba radhi Singida BS haitarajiwi kumchukulia Metacha hatua zaidi.

More Stories

Nyota Geita Gold afunguka rafu ya Aziz KI, Ilikuwa bahati mbaya
Nyota Geita Gold afunguka rafu ya Aziz KI, Ilikuwa bahati mbaya
3h ago
READ MORE →
LAPORTA: Atletico kumuuza Alvarez kwa timu yeyote isipokuwa Barcelona
LAPORTA: Atletico kumuuza Alvarez kwa timu yeyote isipokuwa Barcelona
5h ago
READ MORE →
Ngorongoro Heroes yatangulia nusu fainali CECAFA U20 kwa kishindo
Ngorongoro Heroes yatangulia nusu fainali CECAFA U20 kwa kishindo
7h ago
READ MORE →
Samatta afunga bao lake la pili, Le Havre ikipoteza
Samatta afunga bao lake la pili, Le Havre ikipoteza
7h ago
READ MORE →
Salah hakamatiki Uturuki, apiga hat-trik Trabzonspor ikiifumua Galatasaray 4-0
Salah hakamatiki Uturuki, apiga hat-trik Trabzonspor ikiifumua Galatasaray 4-0
8h ago
READ MORE →
Azam Fc yaonywa, Yanga yakumbana na faini - Kamati ya saa 72
Azam Fc yaonywa, Yanga yakumbana na faini - Kamati ya saa 72
9h ago
READ MORE →
Mshambuliaji wa zamani Yanga aibukia Zambia
Mshambuliaji wa zamani Yanga aibukia Zambia
9h ago
READ MORE →
Barcelona yaendeleza kichapo Laliga ikimfunga Sevilla, Raphinha hashikiki.
Barcelona yaendeleza kichapo Laliga ikimfunga Sevilla, Raphinha hashikiki.
17h ago
READ MORE →
Mamelodi Sundowns yaibuka kidedea mbele ya Al Ahli
Mamelodi Sundowns yaibuka kidedea mbele ya Al Ahli
21h ago
READ MORE →
Arsenal yaduwazwa 3-0 na Brighton
Arsenal yaduwazwa 3-0 na Brighton
21h ago
READ MORE →