International,Transfer News,Atletico Madrid, Barcelona, PSG

Alvarez azidi kuiweka gizani Atletico Madrid

Joel JJ By Joel JJ
25 May 2026
Alvarez azidi kuiweka gizani Atletico Madrid

Mshambuliaji wa kimataifa wa Argentina, Julián Álvarez, hana mpango wa kuongeza mkataba mpya na Atlético Madrid kwa sasa licha ya taarifa zinazoendelea kuhusisha mazungumzo ya kuboresha mkataba wake ndani ya klabu hiyo.

Hatua hiyo imeongeza uvumi kuhusu mustakabali wa nyota huyo wa zamani wa Manchester City, ambaye tayari anawindwa na vigogo mbalimbali wa Ulaya akiwemo FC Barcelona, Paris Saint-Germain pamoja na baadhi ya klabu za Premier League.

Kocha wa Atlético Madrid, Diego Simeone, alizungumza wazi kuhusu hali ya mshambuliaji huyo baada ya mchezo wa mwisho wa La Liga dhidi ya Villarreal, akionyesha kuwa maamuzi ya mchezaji huyo yako mikononi mwake mwenyewe.

“Future ya Álvarez? Hilo si swali langu, ni swali lake. Ana umri wa kutosha kujua anachotaka kufanya na naamini tayari ameshafanya maamuzi yake,” alisema Simeone.

BARCELONA, PSG NA EPL ZAMUWANIA

Taarifa kutoka Hispania na Ufaransa zinaeleza kuwa Barcelona wanaendelea kumtazama Álvarez kama mbadala wa mshambuliaji mkongwe Robert Lewandowski, huku PSG nao wakitajwa kuwa tayari kuingia kwenye vita ya usajili wake.

Aidha, klabu za England zikiwemo Arsenal F.C. zimeonyesha nia ya kumrejesha mshambuliaji huyo Premier League baada ya mafanikio aliyoyapata akiwa Manchester City chini ya Pep Guardiola.

NGUZO MUHIMU ATLETICO

Tangu ajiunge na Atlético Madrid mwaka 2024 akitokea Manchester City kwa ada iliyovunja rekodi ya klabu hiyo, Álvarez amekuwa mmoja wa nyota muhimu ndani ya kikosi cha Simeone.

Msimu huu ameendelea kuonyesha kiwango bora katika La Liga na michuano ya Ulaya, jambo linalofanya Atlético kutokuwa tayari kumuachia kirahisi licha ya presha kutoka kwa vilabu vikubwa Ulaya.

Hata hivyo, kusuasua kwa mazungumzo ya kuongeza mkataba mpya kunaendelea kuongeza uwezekano wa mshambuliaji huyo kuondoka ndani ya dirisha lijalo la usajili.

More Stories

APR Fc yawaondosha aigles du congo kwenye caf champions league
APR Fc yawaondosha aigles du congo kwenye caf champions league
2h ago
READ MORE →
Azam Fc yaomboleza kifo cha mlinda lango U20
Azam Fc yaomboleza kifo cha mlinda lango U20
5h ago
READ MORE →
Hatuna presha kuikabili Yanga - Kocha Gaborone United
Hatuna presha kuikabili Yanga - Kocha Gaborone United
7h ago
READ MORE →
Manqoba aweka tahadhari mechi dhidi ya Gaborone United
Manqoba aweka tahadhari mechi dhidi ya Gaborone United
9h ago
READ MORE →
Rasmi: João Pedro Atwaa Tuzo Ya Mchezaji Bora Wa Mwezi Wa Agosti
Rasmi: João Pedro Atwaa Tuzo Ya Mchezaji Bora Wa Mwezi Wa Agosti
11h ago
READ MORE →
Simba inalenga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, nusu fainali ni lengo kubwa
Simba inalenga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, nusu fainali ni lengo kubwa
11h ago
READ MORE →
Libasse awapiga chini Max na Mwajanga, Kwenye tuzo za Mwezi.
Libasse awapiga chini Max na Mwajanga, Kwenye tuzo za Mwezi.
12h ago
READ MORE →
Fei Toto azipotezea Simba, Yanga
Fei Toto azipotezea Simba, Yanga
14h ago
READ MORE →
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 21, Septemba 11 2026
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 21, Septemba 11 2026
17h ago
READ MORE →
UEFA champions league: matokeo ya usiku
UEFA champions league: matokeo ya usiku
1d ago
READ MORE →