Alvarez azidi kuiweka gizani Atletico Madrid

Joel JJ By Joel JJ • 25th May 2026


Alvarez azidi kuiweka gizani Atletico Madrid

Mshambuliaji wa kimataifa wa Argentina, Julián Álvarez, hana mpango wa kuongeza mkataba mpya na Atlético Madrid kwa sasa licha ya taarifa zinazoendelea kuhusisha mazungumzo ya kuboresha mkataba wake ndani ya klabu hiyo.

Hatua hiyo imeongeza uvumi kuhusu mustakabali wa nyota huyo wa zamani wa Manchester City, ambaye tayari anawindwa na vigogo mbalimbali wa Ulaya akiwemo FC Barcelona, Paris Saint-Germain pamoja na baadhi ya klabu za Premier League.

Kocha wa Atlético Madrid, Diego Simeone, alizungumza wazi kuhusu hali ya mshambuliaji huyo baada ya mchezo wa mwisho wa La Liga dhidi ya Villarreal, akionyesha kuwa maamuzi ya mchezaji huyo yako mikononi mwake mwenyewe.

“Future ya Álvarez? Hilo si swali langu, ni swali lake. Ana umri wa kutosha kujua anachotaka kufanya na naamini tayari ameshafanya maamuzi yake,” alisema Simeone.

BARCELONA, PSG NA EPL ZAMUWANIA

Taarifa kutoka Hispania na Ufaransa zinaeleza kuwa Barcelona wanaendelea kumtazama Álvarez kama mbadala wa mshambuliaji mkongwe Robert Lewandowski, huku PSG nao wakitajwa kuwa tayari kuingia kwenye vita ya usajili wake.

Aidha, klabu za England zikiwemo Arsenal F.C. zimeonyesha nia ya kumrejesha mshambuliaji huyo Premier League baada ya mafanikio aliyoyapata akiwa Manchester City chini ya Pep Guardiola.

NGUZO MUHIMU ATLETICO

Tangu ajiunge na Atlético Madrid mwaka 2024 akitokea Manchester City kwa ada iliyovunja rekodi ya klabu hiyo, Álvarez amekuwa mmoja wa nyota muhimu ndani ya kikosi cha Simeone.

Msimu huu ameendelea kuonyesha kiwango bora katika La Liga na michuano ya Ulaya, jambo linalofanya Atlético kutokuwa tayari kumuachia kirahisi licha ya presha kutoka kwa vilabu vikubwa Ulaya.

Hata hivyo, kusuasua kwa mazungumzo ya kuongeza mkataba mpya kunaendelea kuongeza uwezekano wa mshambuliaji huyo kuondoka ndani ya dirisha lijalo la usajili.


  

More Stories

Azam Fc hiyooo fainali, yaichapa Yanga 3-2 nusu fainali
Azam Fc hiyooo fainali, yaichapa Yanga 3-2 nusu fainali
Today, READ MORE →
Azam Fc 3-2 Yanga, CRDB Cup
Azam Fc 3-2 Yanga, CRDB Cup
Today, READ MORE →
Ni Azam Fc vs Yanga, nani anakwenda fainali kombe la CRDB?
Ni Azam Fc vs Yanga, nani anakwenda fainali kombe la CRDB?
Today, READ MORE →
Liverpool kuongeza dau kumnasa Diomande
Liverpool kuongeza dau kumnasa Diomande
Today, READ MORE →
Prisons wamefufua matumaini kusalia ligi kuu
Prisons wamefufua matumaini kusalia ligi kuu
Today, READ MORE →
Tunisia yaaga kombe la Dunia kwa aibu, yapigwa 4-0 na Japan
Tunisia yaaga kombe la Dunia kwa aibu, yapigwa 4-0 na Japan
Today, READ MORE →
Ivory Coast yapoteza dhidi ya Ujerumani dakika za jioni
Ivory Coast yapoteza dhidi ya Ujerumani dakika za jioni
Today, READ MORE →
Real Madrid yakana kuwasiliana na Olise, wakala wake
Real Madrid yakana kuwasiliana na Olise, wakala wake
Yesterday, READ MORE →
Simba 4-0 Coastal Union, CRDB Cup
Simba 4-0 Coastal Union, CRDB Cup
Yesterday, READ MORE →
Simba yaifumua Coastal Union 4-0, yatinga fainali ya CRDB Bank Cup
Simba yaifumua Coastal Union 4-0, yatinga fainali ya CRDB Bank Cup
Yesterday, READ MORE →