Fei Toto ameshindikana, apewe tuzo yake mapema

Joel JJ By Joel JJ β€’ 26th May 2026


Fei Toto ameshindikana, apewe tuzo yake mapema

Jana Azam FC iliendeleza ubabe uwanja wa Azam Complex wakiwachapa vibnde KMC mabao 3-0 katika mchezo wa ligi kuu ya NBC.

Mabao ya Azam Fc katika mchezo huo yalifungwa na Feisal Saum 'Fei Toto' aliyefunga mabao mawili huku bao la tatu likifungwa na Yoro Diaby.

Fei Toto ameendelea kuwa mtambo wa kuzalisha mabao katika kikosi cha Azam Fc msimu huu akiwa tayari amehusika katika mabao 22.

Amefunga mabao 14 na kutoa pasi nane za usaidizi wa mabao. Mchezaji anayemfuatia ni Allan Okello wa Yanga ambaye amefunga mabao 11 na pasi 7 za usaidizi wa mabao akiwa amehusika kwenye mabao 17.

Ni wazi kama ligi inamalizika leo, Fei Toto anastahili tuzo ya mchezaji bora wa msimu 'MVP' na ufungaji bora pia.

Ni msimu wa tatu mfululizo Fei Toto ameendelea kuwa mtambo wa kuzalisha mabao Azam FC.


  

More Stories

Azam Fc hiyooo fainali, yaichapa Yanga 3-2 nusu fainali
Azam Fc hiyooo fainali, yaichapa Yanga 3-2 nusu fainali
Today, READ MORE β†’
Azam Fc 3-2 Yanga, CRDB Cup
Azam Fc 3-2 Yanga, CRDB Cup
Today, READ MORE β†’
Ni Azam Fc vs Yanga, nani anakwenda fainali kombe la CRDB?
Ni Azam Fc vs Yanga, nani anakwenda fainali kombe la CRDB?
Today, READ MORE β†’
Liverpool kuongeza dau kumnasa Diomande
Liverpool kuongeza dau kumnasa Diomande
Today, READ MORE β†’
Prisons wamefufua matumaini kusalia ligi kuu
Prisons wamefufua matumaini kusalia ligi kuu
Today, READ MORE β†’
Tunisia yaaga kombe la Dunia kwa aibu, yapigwa 4-0 na Japan
Tunisia yaaga kombe la Dunia kwa aibu, yapigwa 4-0 na Japan
Today, READ MORE β†’
Ivory Coast yapoteza dhidi ya Ujerumani dakika za jioni
Ivory Coast yapoteza dhidi ya Ujerumani dakika za jioni
Today, READ MORE β†’
Real Madrid yakana kuwasiliana na Olise, wakala wake
Real Madrid yakana kuwasiliana na Olise, wakala wake
Yesterday, READ MORE β†’
Simba 4-0 Coastal Union, CRDB Cup
Simba 4-0 Coastal Union, CRDB Cup
Yesterday, READ MORE β†’
Simba yaifumua Coastal Union 4-0, yatinga fainali ya CRDB Bank Cup
Simba yaifumua Coastal Union 4-0, yatinga fainali ya CRDB Bank Cup
Yesterday, READ MORE β†’