International,Transfer News,Tottenham, Manchester City, Newcastle

Spurs warudi kwa Savinho

Joel JJ By Joel JJ
β€’
26 May 2026
Spurs warudi kwa Savinho

Baada ya msimu mgumu uliowaweka karibu na eneo la kushuka daraja, Tottenham Hotspur wameanza harakati za kurejesha makali yao kwa kuangalia soko la usajili mapema, wakilenga kuimarisha safu ya ushambuliaji kuelekea msimu ujao.

Kwa mujibu wa mwanahabari wa usajili wa soka, Fabrizio Romano, Spurs wamefufua tena nia yao ya kumsajili winga wa Brazil, Savinho, ambaye kwa sasa anaitumikia Manchester City.

Romano ameripoti kuwa Tottenham wanamfuatilia tena Savinho katika dirisha la usajili la kiangazi, baada ya mazungumzo ya awali kuvunjika mwaka 2025. Winga huyo alikuwa karibu kujiunga na Spurs mwaka mmoja uliopita, lakini Manchester City walizuia uhamisho huo.

Hata hivyo, hali ya sasa inaonyesha kuwa uwezekano wa kuondoka kwake Etihad uko wazi zaidi, huku mazungumzo ya awali kati ya pande husika yakianza tena. Inasemekana Savinho mwenyewe yuko tayari kwa changamoto mpya na anavutiwa na mradi wa Tottenham unaoendelea kujengwa upya.

Zaidi ya Spurs, klabu ya Newcastle United pia inaripotiwa kumfuatilia kwa karibu winga huyo wa Brazil, jambo linaloongeza ushindani katika mbio za kumsaini.

Ripoti hizo pia zinaeleza kuwa kocha Roberto De Zerbi anavutiwa sana na Savinho, akimuhitaji katika kikosi chake ambacho msimu ulioisha kimemaliza nafasi ya 17.

More Stories

Ngorongoro Heroes yatangulia nusu fainali CECAFA U20 kwa kishindo
Ngorongoro Heroes yatangulia nusu fainali CECAFA U20 kwa kishindo
27m ago
READ MORE β†’
Samatta afunga bao lake la pili, Le Havre ikipoteza
Samatta afunga bao lake la pili, Le Havre ikipoteza
28m ago
READ MORE β†’
Salah hakamatiki Uturuki, apiga hat-trik Trabzonspor ikiifumua Galatasaray 4-0
Salah hakamatiki Uturuki, apiga hat-trik Trabzonspor ikiifumua Galatasaray 4-0
1h ago
READ MORE β†’
Azam Fc yaonywa, Yanga yakumbana na faini - Kamati ya saa 72
Azam Fc yaonywa, Yanga yakumbana na faini - Kamati ya saa 72
1h ago
READ MORE β†’
Mshambuliaji wa zamani Yanga aibukia Zambia
Mshambuliaji wa zamani Yanga aibukia Zambia
2h ago
READ MORE β†’
Barcelona yaendeleza kichapo Laliga ikimfunga Sevilla, Raphinha hashikiki.
Barcelona yaendeleza kichapo Laliga ikimfunga Sevilla, Raphinha hashikiki.
9h ago
READ MORE β†’
Mamelodi Sundowns yaibuka kidedea mbele ya Al Ahli
Mamelodi Sundowns yaibuka kidedea mbele ya Al Ahli
14h ago
READ MORE β†’
Arsenal yaduwazwa 3-0 na Brighton
Arsenal yaduwazwa 3-0 na Brighton
14h ago
READ MORE β†’
Nyota Stars waingia kambini tayari kwa mechi za kufuzu Afcon 2027
Nyota Stars waingia kambini tayari kwa mechi za kufuzu Afcon 2027
16h ago
READ MORE β†’
Simba kujichimbia Afrika Kusini kujiandaa na Kariakoo Derby
Simba kujichimbia Afrika Kusini kujiandaa na Kariakoo Derby
16h ago
READ MORE β†’