Local,Normal News,Ligi Kuu, Singida, Mbeya, Prison, Pamba

Singida BS yaifumua Mbeya City, wakati Prisons ikifufukia kwa Pamba Jiji

Joel JJ By Joel JJ
β€’
26 May 2026
Singida BS yaifumua Mbeya City, wakati Prisons ikifufukia kwa Pamba Jiji

Michezo miwili ya Ligi Kuu ya NBC imepigwa leo Jumanne, Mei 26, kukamilisha mechi za mzunguuko wa 25.

Katika Uwanja wa CCM Kirumba mjini Mwanza, Tanzania Prisons waliibuka na ushindi muhimu wa mabao 3-1 dhidi ya Pamba Jiji FC, matokeo yaliyoongeza matumaini ya timu hiyo kujinasua kwenye hatari ya kushuka daraja.

Ushindi huo umeifanya Prisons kuendelea kupambana kusalia ndani ya NBC Premier League huku wakionyesha ari mpya katika hatua za mwisho za msimu.

Wakati huo huo mkoani Singida, Singida Black Stars waliendelea na kiwango bora baada ya kuichapa Mbeya City FC mabao 4-1 kwenye Uwanja wa Airtel.

Mbeya City ndio waliokuwa wa kwanza kupata bao kupitia bao la kujifunga dakika ya nne, lakini Singida Black Stars walirejea kwa nguvu na kusawazisha kupitia Ande Cirille dakika ya 16 kabla ya Malanga Horso Mwaku kufunga bao la pili dakika ya 18. Kipindi cha pili, Khalid Aucho aliongeza bao la tatu kwa mkwaju wa penalti dakika ya 84 kabla ya Malanga kufunga tena dakika ya 89 kuhitimisha ushindi wa mabao 4-1.

Matokeo hayo yameifanya Singida Black Stars kujiimarisha katika nafasi ya nne kwenye msimamo wa ligi, hatua inayoongeza matumaini yao ya kumaliza msimu kwenye nafasi nzuri ya ushindani wa kimataifa.

Kwa upande mwingine, hali imeendelea kuwa mbaya kwa Mbeya City ambao bado wanabaki kwenye eneo la hatari la kucheza play-off ya kushuka daraja. Kipigo hicho kimeongeza presha kwa timu hiyo kuelekea michezo ya mwisho ya msimu huku mashabiki wakianza kuwa na hofu ya hatma yao kwenye ligi kuu.

More Stories

APR Fc yawaondosha aigles du congo kwenye caf champions league
APR Fc yawaondosha aigles du congo kwenye caf champions league
6h ago
READ MORE β†’
Azam Fc yaomboleza kifo cha mlinda lango U20
Azam Fc yaomboleza kifo cha mlinda lango U20
10h ago
READ MORE β†’
Hatuna presha kuikabili Yanga - Kocha Gaborone United
Hatuna presha kuikabili Yanga - Kocha Gaborone United
11h ago
READ MORE β†’
Manqoba aweka tahadhari mechi dhidi ya Gaborone United
Manqoba aweka tahadhari mechi dhidi ya Gaborone United
13h ago
READ MORE β†’
Rasmi: JoΓ£o Pedro Atwaa Tuzo Ya Mchezaji Bora Wa Mwezi Wa Agosti
Rasmi: JoΓ£o Pedro Atwaa Tuzo Ya Mchezaji Bora Wa Mwezi Wa Agosti
16h ago
READ MORE β†’
Simba inalenga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, nusu fainali ni lengo kubwa
Simba inalenga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, nusu fainali ni lengo kubwa
16h ago
READ MORE β†’
Libasse awapiga chini Max na Mwajanga, Kwenye tuzo za Mwezi.
Libasse awapiga chini Max na Mwajanga, Kwenye tuzo za Mwezi.
16h ago
READ MORE β†’
Fei Toto azipotezea Simba, Yanga
Fei Toto azipotezea Simba, Yanga
18h ago
READ MORE β†’
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 21, Septemba 11 2026
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 21, Septemba 11 2026
22h ago
READ MORE β†’
UEFA champions league: matokeo ya usiku
UEFA champions league: matokeo ya usiku
1d ago
READ MORE β†’