Singida BS yaifumua Mbeya City, wakati Prisons ikifufukia kwa Pamba Jiji

Joel JJ By Joel JJ β€’ 26th May 2026


Singida BS yaifumua Mbeya City, wakati Prisons ikifufukia kwa Pamba Jiji

Michezo miwili ya Ligi Kuu ya NBC imepigwa leo Jumanne, Mei 26, kukamilisha mechi za mzunguuko wa 25.

Katika Uwanja wa CCM Kirumba mjini Mwanza, Tanzania Prisons waliibuka na ushindi muhimu wa mabao 3-1 dhidi ya Pamba Jiji FC, matokeo yaliyoongeza matumaini ya timu hiyo kujinasua kwenye hatari ya kushuka daraja.

Ushindi huo umeifanya Prisons kuendelea kupambana kusalia ndani ya NBC Premier League huku wakionyesha ari mpya katika hatua za mwisho za msimu.

Wakati huo huo mkoani Singida, Singida Black Stars waliendelea na kiwango bora baada ya kuichapa Mbeya City FC mabao 4-1 kwenye Uwanja wa Airtel.

Mbeya City ndio waliokuwa wa kwanza kupata bao kupitia bao la kujifunga dakika ya nne, lakini Singida Black Stars walirejea kwa nguvu na kusawazisha kupitia Ande Cirille dakika ya 16 kabla ya Malanga Horso Mwaku kufunga bao la pili dakika ya 18. Kipindi cha pili, Khalid Aucho aliongeza bao la tatu kwa mkwaju wa penalti dakika ya 84 kabla ya Malanga kufunga tena dakika ya 89 kuhitimisha ushindi wa mabao 4-1.

Matokeo hayo yameifanya Singida Black Stars kujiimarisha katika nafasi ya nne kwenye msimamo wa ligi, hatua inayoongeza matumaini yao ya kumaliza msimu kwenye nafasi nzuri ya ushindani wa kimataifa.

Kwa upande mwingine, hali imeendelea kuwa mbaya kwa Mbeya City ambao bado wanabaki kwenye eneo la hatari la kucheza play-off ya kushuka daraja. Kipigo hicho kimeongeza presha kwa timu hiyo kuelekea michezo ya mwisho ya msimu huku mashabiki wakianza kuwa na hofu ya hatma yao kwenye ligi kuu.


  

More Stories

Azam Fc hiyooo fainali, yaichapa Yanga 3-2 nusu fainali
Azam Fc hiyooo fainali, yaichapa Yanga 3-2 nusu fainali
Today, READ MORE β†’
Azam Fc 3-2 Yanga, CRDB Cup
Azam Fc 3-2 Yanga, CRDB Cup
Today, READ MORE β†’
Ni Azam Fc vs Yanga, nani anakwenda fainali kombe la CRDB?
Ni Azam Fc vs Yanga, nani anakwenda fainali kombe la CRDB?
Today, READ MORE β†’
Liverpool kuongeza dau kumnasa Diomande
Liverpool kuongeza dau kumnasa Diomande
Today, READ MORE β†’
Prisons wamefufua matumaini kusalia ligi kuu
Prisons wamefufua matumaini kusalia ligi kuu
Today, READ MORE β†’
Tunisia yaaga kombe la Dunia kwa aibu, yapigwa 4-0 na Japan
Tunisia yaaga kombe la Dunia kwa aibu, yapigwa 4-0 na Japan
Today, READ MORE β†’
Ivory Coast yapoteza dhidi ya Ujerumani dakika za jioni
Ivory Coast yapoteza dhidi ya Ujerumani dakika za jioni
Today, READ MORE β†’
Real Madrid yakana kuwasiliana na Olise, wakala wake
Real Madrid yakana kuwasiliana na Olise, wakala wake
Yesterday, READ MORE β†’
Simba 4-0 Coastal Union, CRDB Cup
Simba 4-0 Coastal Union, CRDB Cup
Yesterday, READ MORE β†’
Simba yaifumua Coastal Union 4-0, yatinga fainali ya CRDB Bank Cup
Simba yaifumua Coastal Union 4-0, yatinga fainali ya CRDB Bank Cup
Yesterday, READ MORE β†’