International,Transfer News,Barcelona, Newcastle, Local

Barcelona hawatanii: Wamnasa Anthony Gordon katika dili la Euro milioni 70

Joel JJ By Joel JJ
β€’
28 May 2026
Barcelona hawatanii: Wamnasa Anthony Gordon katika dili la Euro milioni 70

FC Barcelona wanaendelea kuonyesha kwamba msimu huu wa usajili hawako tayari kufanya mzaha. Klabu hiyo ya Catalonia sasa iko hatua kubwa karibu kumsajili nyota wa Newcastle United, Anthony Gordon, katika dili linalokadiriwa kufikia zaidi ya €70 milioni.

Kwa mujibu wa taarifa, Barcelona na Newcastle wamefikia makubaliano ya awali kuhusu ada ya uhamisho, huku mchezaji huyo akishafikia pia makubaliano binafsi na klabu hiyo ya Hispania.

Ripoti zinaeleza kuwa Gordon anatarajiwa kufanyiwa vipimo vya afya Barcelona kabla ya kukamilisha uhamisho wake, jambo linaloashiria kuwa dili hilo limeingia hatua za mwisho. Barcelona wamekuwa wakimfuatilia mchezaji huyo kwa muda kutokana na uwezo wake wa kucheza pembeni na pia kuongeza kasi ya mashambulizi.

Sababu kuu inayowavutia Barcelona ni uwezo wa Gordon kucheza kwa intensity kubwa, kasi ya kushambulia, na flexibility ya kucheza nafasi mbalimbali za mbele. Kocha Hansi Flick anaamini mchezaji huyo anaweza kusaidia kuongeza nguvu kwenye safu ya ushambuliaji pamoja na kuwa mbadala wa haraka wa wachezaji kama Raphinha.

Kwa upande wa Newcastle, uamuzi wa kumuuza Gordon unaonekana kuwa sehemu ya mpango wa kuimarisha kikosi kwa fedha kubwa zitakazotokana na mauzo hayo, hasa baada ya msimu wenye matokeo yasiyo thabiti kwa klabu hiyo.

Hata hivyo, ingawa makubaliano yanaonekana kuwa karibu kukamilika, hatua za mwisho kama vipimo vya afya na kusaini mkataba bado zinahitajika kabla ya kutangazwa rasmi.

Kilicho wazi ni kwamba Barcelona hawatanii, wanajenga kikosi chenye kasi, nguvu na ubora wa muda mrefu, na Anthony Gordon anaonekana kuwa sehemu muhimu ya mipango hiyo mpya ya Camp Nou.

More Stories

Barcelona yaendeleza kichapo Laliga ikimfunga Sevilla, Raphinha hashikiki.
Barcelona yaendeleza kichapo Laliga ikimfunga Sevilla, Raphinha hashikiki.
2h ago
READ MORE β†’
Mamelodi Sundowns yaibuka kidedea mbele ya Al Ahli
Mamelodi Sundowns yaibuka kidedea mbele ya Al Ahli
6h ago
READ MORE β†’
Arsenal yaduwazwa 3-0 na Brighton
Arsenal yaduwazwa 3-0 na Brighton
7h ago
READ MORE β†’
Nyota Stars waingia kambini tayari kwa mechi za kufuzu Afcon 2027
Nyota Stars waingia kambini tayari kwa mechi za kufuzu Afcon 2027
9h ago
READ MORE β†’
Simba kujichimbia Afrika Kusini kujiandaa na Kariakoo Derby
Simba kujichimbia Afrika Kusini kujiandaa na Kariakoo Derby
9h ago
READ MORE β†’
Madrid Derby: Atletico na Real kwenye vita ya majirani
Madrid Derby: Atletico na Real kwenye vita ya majirani
13h ago
READ MORE β†’
Hii hapa rekodi tamu ya Barker Ligi Kuu
Hii hapa rekodi tamu ya Barker Ligi Kuu
15h ago
READ MORE β†’
Sundowns kuchuana na Al Ahli katika vita ya Afrika na Asia
Sundowns kuchuana na Al Ahli katika vita ya Afrika na Asia
15h ago
READ MORE β†’
Ft: Yanga 1-0 St George, Yanga yapata ushindi mechi ya kirafiki.
Ft: Yanga 1-0 St George, Yanga yapata ushindi mechi ya kirafiki.
1d ago
READ MORE β†’
Dockers Derby yarudi baada ya miaka 14, Ulinzi wa London ukiimarishwa.
Dockers Derby yarudi baada ya miaka 14, Ulinzi wa London ukiimarishwa.
1d ago
READ MORE β†’