Azam Fc yampigia hesabu kali kocha wa zamani Yanga amrithi Ibenge

Joel JJ By Joel JJ • 28th May 2026


Azam Fc yampigia hesabu kali kocha wa zamani Yanga amrithi Ibenge

Uongozi wa klabu ya Azam FC unatajwa kuwa kwenye hatua za awali za mazungumzo na aliyekuwa kocha wa Young Africans SC, Pedro Gonçalves, ili aweze kuinoa timu hiyo kuelekea msimu ujao wa mashindano.

Taarifa zinaeleza kuwa Azam FC inamsaka mbadala wa Florent Ibenge, ambaye amefikia makubaliano na Shirikisho la Soka la Mali kwenda kuinoa timu ya taifa ya nchi hiyo.

Tangu alipoachana na Yanga, Gonçalves bado hajapata klabu au timu nyingine ya kuinoa. Hali hiyo imezidi kuongeza uwezekano wa kocha huyo kujiunga na Wanalambalamba hao wa Azam FC ikiwa mazungumzo yatafanikiwa.

Historia yake Yanga

Young Africans SC iliachana na Gonçalves mapema mwezi huu, mara baada ya mchezo dhidi ya KMC ambao Yanga iliibuka na ushindi wa bao 1-0.

Licha ya kutopoteza mchezo wowote wa ligi katika kipindi chote alichokuwa akiinoa Yanga, uongozi wa klabu hiyo uliamua kumtoa kutokana na kile kilichoelezwa kuwa mbinu zake hazikuendana na falsafa ya soka la timu hiyo.

Azam FC kuimarisha kikosi

Azam FC inaonekana kuingia sokoni kwa nguvu kubwa, ikilenga kupata kocha mwenye uzoefu wa kimataifa ili kuimarisha kikosi chake na kuongeza ushindani dhidi ya vigogo wa ligi kuu nchini Yanga na Simba.

Iwapo mazungumzo yatakamilika, Gonçalves atakuwa mmoja wa makocha waliowahi kuzinoa timu mbili kubwa zinazoshindana vikali kwenye Ligi Kuu Tanzania Bara, jambo linaloweza kuleta msisimko mpya kwenye ligi.


  

More Stories

Azam Fc hiyooo fainali, yaichapa Yanga 3-2 nusu fainali
Azam Fc hiyooo fainali, yaichapa Yanga 3-2 nusu fainali
Today, READ MORE →
Azam Fc 3-2 Yanga, CRDB Cup
Azam Fc 3-2 Yanga, CRDB Cup
Today, READ MORE →
Ni Azam Fc vs Yanga, nani anakwenda fainali kombe la CRDB?
Ni Azam Fc vs Yanga, nani anakwenda fainali kombe la CRDB?
Today, READ MORE →
Liverpool kuongeza dau kumnasa Diomande
Liverpool kuongeza dau kumnasa Diomande
Today, READ MORE →
Prisons wamefufua matumaini kusalia ligi kuu
Prisons wamefufua matumaini kusalia ligi kuu
Today, READ MORE →
Tunisia yaaga kombe la Dunia kwa aibu, yapigwa 4-0 na Japan
Tunisia yaaga kombe la Dunia kwa aibu, yapigwa 4-0 na Japan
Today, READ MORE →
Ivory Coast yapoteza dhidi ya Ujerumani dakika za jioni
Ivory Coast yapoteza dhidi ya Ujerumani dakika za jioni
Today, READ MORE →
Real Madrid yakana kuwasiliana na Olise, wakala wake
Real Madrid yakana kuwasiliana na Olise, wakala wake
Yesterday, READ MORE →
Simba 4-0 Coastal Union, CRDB Cup
Simba 4-0 Coastal Union, CRDB Cup
Yesterday, READ MORE →
Simba yaifumua Coastal Union 4-0, yatinga fainali ya CRDB Bank Cup
Simba yaifumua Coastal Union 4-0, yatinga fainali ya CRDB Bank Cup
Yesterday, READ MORE →