Uongozi wa klabu ya Azam FC unatajwa kuwa kwenye hatua za awali za mazungumzo na aliyekuwa kocha wa Young Africans SC, Pedro Gonçalves, ili aweze kuinoa timu hiyo kuelekea msimu ujao wa mashindano.
Taarifa zinaeleza kuwa Azam FC inamsaka mbadala wa Florent Ibenge, ambaye amefikia makubaliano na Shirikisho la Soka la Mali kwenda kuinoa timu ya taifa ya nchi hiyo.





