Manara kuzisemea timu zote za Taifa Tanzania

Joel JJ By Joel JJ β€’ 28th May 2026


Manara kuzisemea timu zote za Taifa Tanzania

Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mh. Paul Makonda, amemteua Haji Manara kuwa msemaji wa timu zote za Taifa za Tanzania katika hatua inayolenga kuboresha mawasiliano na uhamasishaji wa michezo nchini.

Akizungumza na waandishi wa habari leo Mei 28, 2026 katika Viwanja vya Bunge jijini Dodoma, Waziri Makonda amesema uteuzi huo unalenga kuongeza nguvu katika usimamizi wa taswira na taarifa za timu za Taifa, hususan timu ya Taifa ya mpira wa miguu ya Tanzania.

Mh Makonda amesema Haji Manara atafanya kazi chini ya Baraza la Michezo la Taifa (BMT), ambalo litasimamia utekelezaji wa majukumu yake katika kuratibu Mawasiliano ya timu zote za Taifa.

Lengo la uteuzi

Makonda amesema lengo kuu la uteuzi huo ni kuhakikisha taarifa za timu za Taifa zinawafikia wananchi kwa wakati, kwa uwazi na kwa ufanisi zaidi, pamoja na kuongeza hamasa kwa mashabiki kuelekea mashindano mbalimbali ya kimataifa.

Aidha, uteuzi huo unahusisha timu zote za Taifa, zikiwemo za vijana na wanawake, chini ya mfumo wa usimamizi wa Baraza la Michezo la Taifa.

Manara amewahi kuzitumikia klabu za Yanga na Simba katika nafasi za usemaji kwa mafanikio makubwa.Β 


  

More Stories

Azam Fc hiyooo fainali, yaichapa Yanga 3-2 nusu fainali
Azam Fc hiyooo fainali, yaichapa Yanga 3-2 nusu fainali
Today, READ MORE β†’
Azam Fc 3-2 Yanga, CRDB Cup
Azam Fc 3-2 Yanga, CRDB Cup
Today, READ MORE β†’
Ni Azam Fc vs Yanga, nani anakwenda fainali kombe la CRDB?
Ni Azam Fc vs Yanga, nani anakwenda fainali kombe la CRDB?
Today, READ MORE β†’
Liverpool kuongeza dau kumnasa Diomande
Liverpool kuongeza dau kumnasa Diomande
Today, READ MORE β†’
Prisons wamefufua matumaini kusalia ligi kuu
Prisons wamefufua matumaini kusalia ligi kuu
Today, READ MORE β†’
Tunisia yaaga kombe la Dunia kwa aibu, yapigwa 4-0 na Japan
Tunisia yaaga kombe la Dunia kwa aibu, yapigwa 4-0 na Japan
Today, READ MORE β†’
Ivory Coast yapoteza dhidi ya Ujerumani dakika za jioni
Ivory Coast yapoteza dhidi ya Ujerumani dakika za jioni
Today, READ MORE β†’
Real Madrid yakana kuwasiliana na Olise, wakala wake
Real Madrid yakana kuwasiliana na Olise, wakala wake
Yesterday, READ MORE β†’
Simba 4-0 Coastal Union, CRDB Cup
Simba 4-0 Coastal Union, CRDB Cup
Yesterday, READ MORE β†’
Simba yaifumua Coastal Union 4-0, yatinga fainali ya CRDB Bank Cup
Simba yaifumua Coastal Union 4-0, yatinga fainali ya CRDB Bank Cup
Yesterday, READ MORE β†’