Local,Normal News,Taifa Stars, Yanga, Simba, Azam, Singida, TRA

Manara kuzisemea timu zote za Taifa Tanzania

Joel JJ By Joel JJ
β€’
28 May 2026
Manara kuzisemea timu zote za Taifa Tanzania

Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mh. Paul Makonda, amemteua Haji Manara kuwa msemaji wa timu zote za Taifa za Tanzania katika hatua inayolenga kuboresha mawasiliano na uhamasishaji wa michezo nchini.

Akizungumza na waandishi wa habari leo Mei 28, 2026 katika Viwanja vya Bunge jijini Dodoma, Waziri Makonda amesema uteuzi huo unalenga kuongeza nguvu katika usimamizi wa taswira na taarifa za timu za Taifa, hususan timu ya Taifa ya mpira wa miguu ya Tanzania.

Mh Makonda amesema Haji Manara atafanya kazi chini ya Baraza la Michezo la Taifa (BMT), ambalo litasimamia utekelezaji wa majukumu yake katika kuratibu Mawasiliano ya timu zote za Taifa.

Lengo la uteuzi

Makonda amesema lengo kuu la uteuzi huo ni kuhakikisha taarifa za timu za Taifa zinawafikia wananchi kwa wakati, kwa uwazi na kwa ufanisi zaidi, pamoja na kuongeza hamasa kwa mashabiki kuelekea mashindano mbalimbali ya kimataifa.

Aidha, uteuzi huo unahusisha timu zote za Taifa, zikiwemo za vijana na wanawake, chini ya mfumo wa usimamizi wa Baraza la Michezo la Taifa.

Manara amewahi kuzitumikia klabu za Yanga na Simba katika nafasi za usemaji kwa mafanikio makubwa.Β 

More Stories

APR Fc yawaondosha aigles du congo kwenye caf champions league
APR Fc yawaondosha aigles du congo kwenye caf champions league
1h ago
READ MORE β†’
Azam Fc yaomboleza kifo cha mlinda lango U20
Azam Fc yaomboleza kifo cha mlinda lango U20
4h ago
READ MORE β†’
Hatuna presha kuikabili Yanga - Kocha Gaborone United
Hatuna presha kuikabili Yanga - Kocha Gaborone United
6h ago
READ MORE β†’
Manqoba aweka tahadhari mechi dhidi ya Gaborone United
Manqoba aweka tahadhari mechi dhidi ya Gaborone United
8h ago
READ MORE β†’
Rasmi: JoΓ£o Pedro Atwaa Tuzo Ya Mchezaji Bora Wa Mwezi Wa Agosti
Rasmi: JoΓ£o Pedro Atwaa Tuzo Ya Mchezaji Bora Wa Mwezi Wa Agosti
10h ago
READ MORE β†’
Simba inalenga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, nusu fainali ni lengo kubwa
Simba inalenga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, nusu fainali ni lengo kubwa
11h ago
READ MORE β†’
Libasse awapiga chini Max na Mwajanga, Kwenye tuzo za Mwezi.
Libasse awapiga chini Max na Mwajanga, Kwenye tuzo za Mwezi.
11h ago
READ MORE β†’
Fei Toto azipotezea Simba, Yanga
Fei Toto azipotezea Simba, Yanga
13h ago
READ MORE β†’
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 21, Septemba 11 2026
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 21, Septemba 11 2026
16h ago
READ MORE β†’
UEFA champions league: matokeo ya usiku
UEFA champions league: matokeo ya usiku
1d ago
READ MORE β†’