International,Transfer News,Chelsea, Real Madrid, Manchester City, PSG

Enzo aiwekea ngumu Chelsea, ataka kuondoka

Joel JJ By Joel JJ
28 May 2026
Enzo aiwekea ngumu Chelsea, ataka kuondoka

Kiungo wa kimataifa wa Argentina, Enzo Fernández, ameweka wazi msimamo wake wa kutaka kuondoka katika klabu ya Chelsea FC katika dirisha lijalo la usajili wa majira ya kiangazi, huku mvutano kati ya pande hizo mbili ukizidi kuongezeka.

Kwa mujibu wa taarifa za karibu, Chelsea imeweka dau kubwa la takribani pauni milioni 120 (zaidi ya shilingi bilioni 390) ili kumruhusu mchezaji huyo kuondoka, hatua inayoonyesha dhamira ya klabu kutotaka kumpoteza kwa bei ya chini.

Vilabu vikubwa Ulaya vamuandama

Hali ya Enzo imevuta hisia za mabingwa na vigogo wa soka barani Ulaya, ambapo klabu za Real Madrid, Manchester City na Paris Saint-Germain zimeanza kufuatilia kwa karibu mwenendo wa kiungo huyo mwenye umri wa miaka 25.

Vilabu hivyo vinaaminika kumwona Enzo kama kiungo muhimu anayeweza kuimarisha safu ya kati kutokana na uwezo wake wa kupiga pasi, kudhibiti mchezo na kuchangia mabao.

Uhusiano na Chelsea wazidi kuzorota

Chanzo cha karibu kimeeleza kuwa uhusiano kati ya Enzo na Chelsea umeanza kuyumba, hasa baada ya mchezaji huyo kufungiwa mechi mbili mapema msimu huu kutokana na tukio lililotafsiriwa kama vitendo vya “kujipendekeza” kwa Real Madrid wakati wa mapumziko ya mechi za kimataifa mwezi Machi.

Tukio hilo limeongeza mvutano ndani ya klabu na kuchochea tetesi za kuhitaji mabadiliko ya mazingira kwa mchezaji huyo.

Mazungumzo ya mkataba yagonga mwamba

Mazungumzo ya kuongeza mkataba kati ya Chelsea FC na wakala wake, Javier Pastore, yameelezwa kugonga mwamba kutokana na Enzo kutoridhishwa na masuala ya mshahara pamoja na masharti ya kifedha yaliyowekwa na klabu.

Hali hii imeacha mlango wazi kwa klabu nyingine kuingia katika mbio za kumsajili.

More Stories

APR Fc yawaondosha aigles du congo kwenye caf champions league
APR Fc yawaondosha aigles du congo kwenye caf champions league
5h ago
READ MORE →
Azam Fc yaomboleza kifo cha mlinda lango U20
Azam Fc yaomboleza kifo cha mlinda lango U20
8h ago
READ MORE →
Hatuna presha kuikabili Yanga - Kocha Gaborone United
Hatuna presha kuikabili Yanga - Kocha Gaborone United
10h ago
READ MORE →
Manqoba aweka tahadhari mechi dhidi ya Gaborone United
Manqoba aweka tahadhari mechi dhidi ya Gaborone United
12h ago
READ MORE →
Rasmi: João Pedro Atwaa Tuzo Ya Mchezaji Bora Wa Mwezi Wa Agosti
Rasmi: João Pedro Atwaa Tuzo Ya Mchezaji Bora Wa Mwezi Wa Agosti
14h ago
READ MORE →
Simba inalenga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, nusu fainali ni lengo kubwa
Simba inalenga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, nusu fainali ni lengo kubwa
15h ago
READ MORE →
Libasse awapiga chini Max na Mwajanga, Kwenye tuzo za Mwezi.
Libasse awapiga chini Max na Mwajanga, Kwenye tuzo za Mwezi.
15h ago
READ MORE →
Fei Toto azipotezea Simba, Yanga
Fei Toto azipotezea Simba, Yanga
17h ago
READ MORE →
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 21, Septemba 11 2026
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 21, Septemba 11 2026
20h ago
READ MORE →
UEFA champions league: matokeo ya usiku
UEFA champions league: matokeo ya usiku
1d ago
READ MORE →