Enzo aiwekea ngumu Chelsea, ataka kuondoka

Joel JJ By Joel JJ • 28th May 2026


Enzo aiwekea ngumu Chelsea, ataka kuondoka

Kiungo wa kimataifa wa Argentina, Enzo Fernández, ameweka wazi msimamo wake wa kutaka kuondoka katika klabu ya Chelsea FC katika dirisha lijalo la usajili wa majira ya kiangazi, huku mvutano kati ya pande hizo mbili ukizidi kuongezeka.

Kwa mujibu wa taarifa za karibu, Chelsea imeweka dau kubwa la takribani pauni milioni 120 (zaidi ya shilingi bilioni 390) ili kumruhusu mchezaji huyo kuondoka, hatua inayoonyesha dhamira ya klabu kutotaka kumpoteza kwa bei ya chini.

Vilabu vikubwa Ulaya vamuandama

Hali ya Enzo imevuta hisia za mabingwa na vigogo wa soka barani Ulaya, ambapo klabu za Real Madrid, Manchester City na Paris Saint-Germain zimeanza kufuatilia kwa karibu mwenendo wa kiungo huyo mwenye umri wa miaka 25.

Vilabu hivyo vinaaminika kumwona Enzo kama kiungo muhimu anayeweza kuimarisha safu ya kati kutokana na uwezo wake wa kupiga pasi, kudhibiti mchezo na kuchangia mabao.

Uhusiano na Chelsea wazidi kuzorota

Chanzo cha karibu kimeeleza kuwa uhusiano kati ya Enzo na Chelsea umeanza kuyumba, hasa baada ya mchezaji huyo kufungiwa mechi mbili mapema msimu huu kutokana na tukio lililotafsiriwa kama vitendo vya “kujipendekeza” kwa Real Madrid wakati wa mapumziko ya mechi za kimataifa mwezi Machi.

Tukio hilo limeongeza mvutano ndani ya klabu na kuchochea tetesi za kuhitaji mabadiliko ya mazingira kwa mchezaji huyo.

Mazungumzo ya mkataba yagonga mwamba

Mazungumzo ya kuongeza mkataba kati ya Chelsea FC na wakala wake, Javier Pastore, yameelezwa kugonga mwamba kutokana na Enzo kutoridhishwa na masuala ya mshahara pamoja na masharti ya kifedha yaliyowekwa na klabu.

Hali hii imeacha mlango wazi kwa klabu nyingine kuingia katika mbio za kumsajili.


  

More Stories

Azam Fc hiyooo fainali, yaichapa Yanga 3-2 nusu fainali
Azam Fc hiyooo fainali, yaichapa Yanga 3-2 nusu fainali
Today, READ MORE →
Azam Fc 3-2 Yanga, CRDB Cup
Azam Fc 3-2 Yanga, CRDB Cup
Today, READ MORE →
Ni Azam Fc vs Yanga, nani anakwenda fainali kombe la CRDB?
Ni Azam Fc vs Yanga, nani anakwenda fainali kombe la CRDB?
Today, READ MORE →
Liverpool kuongeza dau kumnasa Diomande
Liverpool kuongeza dau kumnasa Diomande
Today, READ MORE →
Prisons wamefufua matumaini kusalia ligi kuu
Prisons wamefufua matumaini kusalia ligi kuu
Today, READ MORE →
Tunisia yaaga kombe la Dunia kwa aibu, yapigwa 4-0 na Japan
Tunisia yaaga kombe la Dunia kwa aibu, yapigwa 4-0 na Japan
Today, READ MORE →
Ivory Coast yapoteza dhidi ya Ujerumani dakika za jioni
Ivory Coast yapoteza dhidi ya Ujerumani dakika za jioni
Today, READ MORE →
Real Madrid yakana kuwasiliana na Olise, wakala wake
Real Madrid yakana kuwasiliana na Olise, wakala wake
Yesterday, READ MORE →
Simba 4-0 Coastal Union, CRDB Cup
Simba 4-0 Coastal Union, CRDB Cup
Yesterday, READ MORE →
Simba yaifumua Coastal Union 4-0, yatinga fainali ya CRDB Bank Cup
Simba yaifumua Coastal Union 4-0, yatinga fainali ya CRDB Bank Cup
Yesterday, READ MORE →