Local,Normal News,Belouizdad, Simba

Ahoua mambo magumu CR Belouizdad

Joel JJ By Joel JJ
29 May 2026
Ahoua mambo magumu CR Belouizdad

Baada ya kuondoka kwa kishindo ndani ya Simba SC na kujiunga na klabu ya Algeria, CR Belouizdad, maisha ya kiungo mshambuliaji Jean Charles Ahoua yanaonekana kutokwenda kama alivyotarajia.

Nyota huyo mwenye umri wa miaka 24 sasa ameanza kufikiria mustakabali wake baada ya kushindwa kupata nafasi ya kucheza mara kwa mara ndani ya kikosi hicho.

Ahoua alitambulishwa rasmi na CR Belouizdad mapema mwaka huu kwa mkataba wa miaka miwili na nusu akitokea Simba SC, huku akitajwa kuwa moja ya sajili kubwa za dirisha la usajili wa Januari.

Hata hivyo, mambo yamebadilika kwa kasi ndani ya kikosi hicho cha Algeria. Taarifa zinaeleza kuwa kiungo huyo mshambuliaji hafurahishwi na kuendelea kukaa benchi mara kwa mara, jambo ambalo limeanza kumfanya afikirie kuondoka mwishoni mwa msimu huu licha ya kuwa bado ana mkataba wa miaka miwili zaidi.

Katika mechi tisa za mwisho za CR Belouizdad, Ahoua amepewa dakika moja pekee ya kucheza, hali inayozua maswali juu ya nafasi yake ndani ya mipango ya benchi la ufundi la klabu hiyo.

Wakati akiwasili Algeria, Ahoua alipokelewa kama “silaha mpya” ya timu kutokana na kiwango kikubwa alichoonyesha akiwa Simba SC na matarajio yalikuwa angekuwa nyota muhimu.

Kwa sasa tayari kuna taarifa kuwa taratibu za kusaka timu mpya zimeanza, huku ikielezwa kuwa mchezaji huyo anahitaji sehemu ambayo atapata nafasi ya kucheza mara kwa mara ili kurejesha kiwango chake na kuendelea kukuza kipaji chake.

More Stories

APR Fc yawaondosha aigles du congo kwenye caf champions league
APR Fc yawaondosha aigles du congo kwenye caf champions league
2h ago
READ MORE →
Azam Fc yaomboleza kifo cha mlinda lango U20
Azam Fc yaomboleza kifo cha mlinda lango U20
5h ago
READ MORE →
Hatuna presha kuikabili Yanga - Kocha Gaborone United
Hatuna presha kuikabili Yanga - Kocha Gaborone United
7h ago
READ MORE →
Manqoba aweka tahadhari mechi dhidi ya Gaborone United
Manqoba aweka tahadhari mechi dhidi ya Gaborone United
9h ago
READ MORE →
Rasmi: João Pedro Atwaa Tuzo Ya Mchezaji Bora Wa Mwezi Wa Agosti
Rasmi: João Pedro Atwaa Tuzo Ya Mchezaji Bora Wa Mwezi Wa Agosti
11h ago
READ MORE →
Simba inalenga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, nusu fainali ni lengo kubwa
Simba inalenga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, nusu fainali ni lengo kubwa
11h ago
READ MORE →
Libasse awapiga chini Max na Mwajanga, Kwenye tuzo za Mwezi.
Libasse awapiga chini Max na Mwajanga, Kwenye tuzo za Mwezi.
12h ago
READ MORE →
Fei Toto azipotezea Simba, Yanga
Fei Toto azipotezea Simba, Yanga
14h ago
READ MORE →
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 21, Septemba 11 2026
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 21, Septemba 11 2026
17h ago
READ MORE →
UEFA champions league: matokeo ya usiku
UEFA champions league: matokeo ya usiku
1d ago
READ MORE →