Ahoua mambo magumu CR Belouizdad

Joel JJ By Joel JJ β€’ 29th May 2026


Ahoua mambo magumu CR Belouizdad

Baada ya kuondoka kwa kishindo ndani ya Simba SC na kujiunga na klabu ya Algeria, CR Belouizdad, maisha ya kiungo mshambuliaji Jean Charles Ahoua yanaonekana kutokwenda kama alivyotarajia.

Nyota huyo mwenye umri wa miaka 24 sasa ameanza kufikiria mustakabali wake baada ya kushindwa kupata nafasi ya kucheza mara kwa mara ndani ya kikosi hicho.

Ahoua alitambulishwa rasmi na CR Belouizdad mapema mwaka huu kwa mkataba wa miaka miwili na nusu akitokea Simba SC, huku akitajwa kuwa moja ya sajili kubwa za dirisha la usajili wa Januari.

Hata hivyo, mambo yamebadilika kwa kasi ndani ya kikosi hicho cha Algeria. Taarifa zinaeleza kuwa kiungo huyo mshambuliaji hafurahishwi na kuendelea kukaa benchi mara kwa mara, jambo ambalo limeanza kumfanya afikirie kuondoka mwishoni mwa msimu huu licha ya kuwa bado ana mkataba wa miaka miwili zaidi.

Katika mechi tisa za mwisho za CR Belouizdad, Ahoua amepewa dakika moja pekee ya kucheza, hali inayozua maswali juu ya nafasi yake ndani ya mipango ya benchi la ufundi la klabu hiyo.

Wakati akiwasili Algeria, Ahoua alipokelewa kama β€œsilaha mpya” ya timu kutokana na kiwango kikubwa alichoonyesha akiwa Simba SC na matarajio yalikuwa angekuwa nyota muhimu.

Kwa sasa tayari kuna taarifa kuwa taratibu za kusaka timu mpya zimeanza, huku ikielezwa kuwa mchezaji huyo anahitaji sehemu ambayo atapata nafasi ya kucheza mara kwa mara ili kurejesha kiwango chake na kuendelea kukuza kipaji chake.


  

More Stories

Azam Fc hiyooo fainali, yaichapa Yanga 3-2 nusu fainali
Azam Fc hiyooo fainali, yaichapa Yanga 3-2 nusu fainali
Today, READ MORE β†’
Azam Fc 3-2 Yanga, CRDB Cup
Azam Fc 3-2 Yanga, CRDB Cup
Today, READ MORE β†’
Ni Azam Fc vs Yanga, nani anakwenda fainali kombe la CRDB?
Ni Azam Fc vs Yanga, nani anakwenda fainali kombe la CRDB?
Today, READ MORE β†’
Liverpool kuongeza dau kumnasa Diomande
Liverpool kuongeza dau kumnasa Diomande
Today, READ MORE β†’
Prisons wamefufua matumaini kusalia ligi kuu
Prisons wamefufua matumaini kusalia ligi kuu
Today, READ MORE β†’
Tunisia yaaga kombe la Dunia kwa aibu, yapigwa 4-0 na Japan
Tunisia yaaga kombe la Dunia kwa aibu, yapigwa 4-0 na Japan
Today, READ MORE β†’
Ivory Coast yapoteza dhidi ya Ujerumani dakika za jioni
Ivory Coast yapoteza dhidi ya Ujerumani dakika za jioni
Today, READ MORE β†’
Real Madrid yakana kuwasiliana na Olise, wakala wake
Real Madrid yakana kuwasiliana na Olise, wakala wake
Yesterday, READ MORE β†’
Simba 4-0 Coastal Union, CRDB Cup
Simba 4-0 Coastal Union, CRDB Cup
Yesterday, READ MORE β†’
Simba yaifumua Coastal Union 4-0, yatinga fainali ya CRDB Bank Cup
Simba yaifumua Coastal Union 4-0, yatinga fainali ya CRDB Bank Cup
Yesterday, READ MORE β†’