Mbappe amepishana na gari la mshahara PSG

Joel JJ By Joel JJ • 31st May 2026


Mbappe amepishana na gari la mshahara PSG

Klabu ya Paris Saint-Germain imeendelea kuandika historia mpya barani Ulaya baada ya kutwaa taji la pili mfululizo la UEFA Champions League, kufuatia ushindi wa penalti 4-3 dhidi ya Arsenal FC katika fainali kali iliyochezwa Mei 30, 2026 jijini Budapest.

Mchezo huo uliisha kwa sare ya 1-1 ndani ya dakika 120, kabla ya PSG kuibuka na ubingwa kupitia mikwaju ya penalti, ushindi ambao uliwafanya kuendelea kutawala soka la Ulaya kwa msimu wa pili mfululizo.

Ushindi wa PSG na historia mpya Ulaya

PSG sasa ni moja ya timu chache katika historia ya kisasa ya Champions League kutetea ubingwa wao kwa mafanikio, jambo linalothibitisha mabadiliko makubwa ndani ya klabu hiyo baada ya kujijenga upya.

Ushindi huu pia unaweka PSG katika kundi la vilabu vilivyoonyesha uthabiti mkubwa katika mashindano ya Ulaya, huku mashabiki wao wakisherehekea mafanikio makubwa ya mfululizo.

Hadithi ya Mbappé na Real Madrid

Wakati PSG ikiendelea kung’ara, macho ya dunia ya soka bado yapo kwa nyota wa Ufaransa Kylian Mbappé, ambaye alihamia katika klabu ya Real Madrid CF akiamini kuwa ndiko atakakopata nafasi kubwa ya kushinda tena Champions League na kushinda tuzo ya Ballon d'or.

Hata hivyo, hali imekuwa tofauti, waswahili wanasema amepishana na gari la mshahara..! presha imeendelea kumkabili Madrid kutokana na matarajio makubwa ya mashabiki na matokeo yasiyo thabiti.

Msimu huu Real Madrid haikushinda taji lolote huku takwimu zikionyesha tangu Mbappe atue kwa mabingwa hao wa kihistoria Ulaya, mambo yanawaendelea kombo hadi kupelekea baadhi ya mashabiki kushinikiza aondoke

Mgogoro wa mashabiki Real Madrid

Sehemu kubwa ya mashabiki wa Real Madrid wameonyesha kutoridhishwa na mwenendo wa timu hiyo, wakimtaja Mbappe kama mmoja wa wachezaji wanaoikwamisha timu hiyo wakimuita 'dikteta'

Kampeni ya kutaka Mbappe aondoke Real Madrid imeendeshwa mitandaoni ambapo takribani mashabiki 700M kote Duniani wakisaini petisheni hiyo.


  

More Stories

Azam Fc hiyooo fainali, yaichapa Yanga 3-2 nusu fainali
Azam Fc hiyooo fainali, yaichapa Yanga 3-2 nusu fainali
Today, READ MORE →
Azam Fc 3-2 Yanga, CRDB Cup
Azam Fc 3-2 Yanga, CRDB Cup
Today, READ MORE →
Ni Azam Fc vs Yanga, nani anakwenda fainali kombe la CRDB?
Ni Azam Fc vs Yanga, nani anakwenda fainali kombe la CRDB?
Today, READ MORE →
Liverpool kuongeza dau kumnasa Diomande
Liverpool kuongeza dau kumnasa Diomande
Today, READ MORE →
Prisons wamefufua matumaini kusalia ligi kuu
Prisons wamefufua matumaini kusalia ligi kuu
Today, READ MORE →
Tunisia yaaga kombe la Dunia kwa aibu, yapigwa 4-0 na Japan
Tunisia yaaga kombe la Dunia kwa aibu, yapigwa 4-0 na Japan
Today, READ MORE →
Ivory Coast yapoteza dhidi ya Ujerumani dakika za jioni
Ivory Coast yapoteza dhidi ya Ujerumani dakika za jioni
Today, READ MORE →
Real Madrid yakana kuwasiliana na Olise, wakala wake
Real Madrid yakana kuwasiliana na Olise, wakala wake
Yesterday, READ MORE →
Simba 4-0 Coastal Union, CRDB Cup
Simba 4-0 Coastal Union, CRDB Cup
Yesterday, READ MORE →
Simba yaifumua Coastal Union 4-0, yatinga fainali ya CRDB Bank Cup
Simba yaifumua Coastal Union 4-0, yatinga fainali ya CRDB Bank Cup
Yesterday, READ MORE →