International,Normal News,PSG, Real Madrid

Mbappe amepishana na gari la mshahara PSG

Joel JJ By Joel JJ
31 May 2026
Mbappe amepishana na gari la mshahara PSG

Klabu ya Paris Saint-Germain imeendelea kuandika historia mpya barani Ulaya baada ya kutwaa taji la pili mfululizo la UEFA Champions League, kufuatia ushindi wa penalti 4-3 dhidi ya Arsenal FC katika fainali kali iliyochezwa Mei 30, 2026 jijini Budapest.

Mchezo huo uliisha kwa sare ya 1-1 ndani ya dakika 120, kabla ya PSG kuibuka na ubingwa kupitia mikwaju ya penalti, ushindi ambao uliwafanya kuendelea kutawala soka la Ulaya kwa msimu wa pili mfululizo.

Ushindi wa PSG na historia mpya Ulaya

PSG sasa ni moja ya timu chache katika historia ya kisasa ya Champions League kutetea ubingwa wao kwa mafanikio, jambo linalothibitisha mabadiliko makubwa ndani ya klabu hiyo baada ya kujijenga upya.

Ushindi huu pia unaweka PSG katika kundi la vilabu vilivyoonyesha uthabiti mkubwa katika mashindano ya Ulaya, huku mashabiki wao wakisherehekea mafanikio makubwa ya mfululizo.

Hadithi ya Mbappé na Real Madrid

Wakati PSG ikiendelea kung’ara, macho ya dunia ya soka bado yapo kwa nyota wa Ufaransa Kylian Mbappé, ambaye alihamia katika klabu ya Real Madrid CF akiamini kuwa ndiko atakakopata nafasi kubwa ya kushinda tena Champions League na kushinda tuzo ya Ballon d'or.

Hata hivyo, hali imekuwa tofauti, waswahili wanasema amepishana na gari la mshahara..! presha imeendelea kumkabili Madrid kutokana na matarajio makubwa ya mashabiki na matokeo yasiyo thabiti.

Msimu huu Real Madrid haikushinda taji lolote huku takwimu zikionyesha tangu Mbappe atue kwa mabingwa hao wa kihistoria Ulaya, mambo yanawaendelea kombo hadi kupelekea baadhi ya mashabiki kushinikiza aondoke

Mgogoro wa mashabiki Real Madrid

Sehemu kubwa ya mashabiki wa Real Madrid wameonyesha kutoridhishwa na mwenendo wa timu hiyo, wakimtaja Mbappe kama mmoja wa wachezaji wanaoikwamisha timu hiyo wakimuita 'dikteta'

Kampeni ya kutaka Mbappe aondoke Real Madrid imeendeshwa mitandaoni ambapo takribani mashabiki 700M kote Duniani wakisaini petisheni hiyo.

More Stories

Manchester City yaichapa Sunderland 5–3 katika mechi ya mabao nane
Manchester City yaichapa Sunderland 5–3 katika mechi ya mabao nane
54m ago
READ MORE →
Atletico yang’ara kwenye dabi, Real Madrid aangukia pua ugenini
Atletico yang’ara kwenye dabi, Real Madrid aangukia pua ugenini
1h ago
READ MORE →
Nyota Geita Gold afunguka rafu ya Aziz KI, Ilikuwa bahati mbaya
Nyota Geita Gold afunguka rafu ya Aziz KI, Ilikuwa bahati mbaya
7h ago
READ MORE →
LAPORTA: Atletico kumuuza Alvarez kwa timu yeyote isipokuwa Barcelona
LAPORTA: Atletico kumuuza Alvarez kwa timu yeyote isipokuwa Barcelona
9h ago
READ MORE →
Ngorongoro Heroes yatangulia nusu fainali CECAFA U20 kwa kishindo
Ngorongoro Heroes yatangulia nusu fainali CECAFA U20 kwa kishindo
11h ago
READ MORE →
Samatta afunga bao lake la pili, Le Havre ikipoteza
Samatta afunga bao lake la pili, Le Havre ikipoteza
11h ago
READ MORE →
Salah hakamatiki Uturuki, apiga hat-trik Trabzonspor ikiifumua Galatasaray 4-0
Salah hakamatiki Uturuki, apiga hat-trik Trabzonspor ikiifumua Galatasaray 4-0
12h ago
READ MORE →
Azam Fc yaonywa, Yanga yakumbana na faini - Kamati ya saa 72
Azam Fc yaonywa, Yanga yakumbana na faini - Kamati ya saa 72
12h ago
READ MORE →
Mshambuliaji wa zamani Yanga aibukia Zambia
Mshambuliaji wa zamani Yanga aibukia Zambia
12h ago
READ MORE →
Barcelona yaendeleza kichapo Laliga ikimfunga Sevilla, Raphinha hashikiki.
Barcelona yaendeleza kichapo Laliga ikimfunga Sevilla, Raphinha hashikiki.
20h ago
READ MORE →