Local,Normal News,Taifa Stars, Azam

Majeraha yamuondoa Fei Toto kikosi cha Stars

Joel JJ By Joel JJ
1 Jun 2026
Majeraha yamuondoa Fei Toto kikosi cha Stars

Kiungo mshambuliaji, Feisal Salum, amekosa nafasi katika kikosi cha timu ya taifa ya Tanzania, baada ya kugundulika kuwa na majeraha yaliyomfanya ashindwe kuendelea na majukumu ya kimataifa.

Kwa mujibu wa Ofisa Habari wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania, Cliford Ndimbo, Fei Toto alifika kambini akiwa ameitwa kwenye kikosi hicho, lakini hali yake ya afya ilibainika kutokuwa sawa.

Ndimbo amesema baada ya mchezaji huyo kufanyiwa uchunguzi wa kina na jopo la madaktari, iligundulika kuwa hataweza kushiriki mechi mbili za kirafiki zilizo mbele ya timu hiyo.

“Baada ya Fei Toto kuwasili kambini alionekana hayuko fiti na alipofanyiwa uchunguzi zaidi jopo la matabibu limeona hatoweza kucheza mechi hizo mbili za kirafiki,” alieleza Ndimbo.

Pamoja na kuondoka kwa Fei Toto kwenye kikosi, Shirikisho halijatangaza mchezaji mwingine kuchukua nafasi yake kwa sasa. Hata hivyo, imeelezwa kuwa endapo kutakuwa na mabadiliko, taarifa rasmi zitatolewa kwa umma.

Stars kuondoka kuelekea Morocco

Katika hatua nyingine, timu ya Taifa ya Tanzania itaondoka leo saa 5:00 usiku kuelekea Morocco kwa ajili ya mechi za kirafiki za kimataifa.

Timu hiyo itacheza dhidi ya Uganda tarehe 5 Juni, kabla ya kumenyana na Rwanda tarehe 9 Juni.

More Stories

APR Fc yawaondosha aigles du congo kwenye caf champions league
APR Fc yawaondosha aigles du congo kwenye caf champions league
2h ago
READ MORE →
Azam Fc yaomboleza kifo cha mlinda lango U20
Azam Fc yaomboleza kifo cha mlinda lango U20
6h ago
READ MORE →
Hatuna presha kuikabili Yanga - Kocha Gaborone United
Hatuna presha kuikabili Yanga - Kocha Gaborone United
8h ago
READ MORE →
Manqoba aweka tahadhari mechi dhidi ya Gaborone United
Manqoba aweka tahadhari mechi dhidi ya Gaborone United
10h ago
READ MORE →
Rasmi: João Pedro Atwaa Tuzo Ya Mchezaji Bora Wa Mwezi Wa Agosti
Rasmi: João Pedro Atwaa Tuzo Ya Mchezaji Bora Wa Mwezi Wa Agosti
12h ago
READ MORE →
Simba inalenga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, nusu fainali ni lengo kubwa
Simba inalenga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, nusu fainali ni lengo kubwa
12h ago
READ MORE →
Libasse awapiga chini Max na Mwajanga, Kwenye tuzo za Mwezi.
Libasse awapiga chini Max na Mwajanga, Kwenye tuzo za Mwezi.
13h ago
READ MORE →
Fei Toto azipotezea Simba, Yanga
Fei Toto azipotezea Simba, Yanga
15h ago
READ MORE →
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 21, Septemba 11 2026
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 21, Septemba 11 2026
18h ago
READ MORE →
UEFA champions league: matokeo ya usiku
UEFA champions league: matokeo ya usiku
1d ago
READ MORE →