Majeraha yamuondoa Fei Toto kikosi cha Stars

Joel JJ By Joel JJ β€’ 1st June 2026


Majeraha yamuondoa Fei Toto kikosi cha Stars

Kiungo mshambuliaji, Feisal Salum, amekosa nafasi katika kikosi cha timu ya taifa ya Tanzania, baada ya kugundulika kuwa na majeraha yaliyomfanya ashindwe kuendelea na majukumu ya kimataifa.

Kwa mujibu wa Ofisa Habari wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania, Cliford Ndimbo, Fei Toto alifika kambini akiwa ameitwa kwenye kikosi hicho, lakini hali yake ya afya ilibainika kutokuwa sawa.

Ndimbo amesema baada ya mchezaji huyo kufanyiwa uchunguzi wa kina na jopo la madaktari, iligundulika kuwa hataweza kushiriki mechi mbili za kirafiki zilizo mbele ya timu hiyo.

β€œBaada ya Fei Toto kuwasili kambini alionekana hayuko fiti na alipofanyiwa uchunguzi zaidi jopo la matabibu limeona hatoweza kucheza mechi hizo mbili za kirafiki,” alieleza Ndimbo.

Pamoja na kuondoka kwa Fei Toto kwenye kikosi, Shirikisho halijatangaza mchezaji mwingine kuchukua nafasi yake kwa sasa. Hata hivyo, imeelezwa kuwa endapo kutakuwa na mabadiliko, taarifa rasmi zitatolewa kwa umma.

Stars kuondoka kuelekea Morocco

Katika hatua nyingine, timu ya Taifa ya Tanzania itaondoka leo saa 5:00 usiku kuelekea Morocco kwa ajili ya mechi za kirafiki za kimataifa.

Timu hiyo itacheza dhidi ya Uganda tarehe 5 Juni, kabla ya kumenyana na Rwanda tarehe 9 Juni.


  

More Stories

Azam Fc hiyooo fainali, yaichapa Yanga 3-2 nusu fainali
Azam Fc hiyooo fainali, yaichapa Yanga 3-2 nusu fainali
Today, READ MORE β†’
Azam Fc 3-2 Yanga, CRDB Cup
Azam Fc 3-2 Yanga, CRDB Cup
Today, READ MORE β†’
Ni Azam Fc vs Yanga, nani anakwenda fainali kombe la CRDB?
Ni Azam Fc vs Yanga, nani anakwenda fainali kombe la CRDB?
Today, READ MORE β†’
Liverpool kuongeza dau kumnasa Diomande
Liverpool kuongeza dau kumnasa Diomande
Today, READ MORE β†’
Prisons wamefufua matumaini kusalia ligi kuu
Prisons wamefufua matumaini kusalia ligi kuu
Today, READ MORE β†’
Tunisia yaaga kombe la Dunia kwa aibu, yapigwa 4-0 na Japan
Tunisia yaaga kombe la Dunia kwa aibu, yapigwa 4-0 na Japan
Today, READ MORE β†’
Ivory Coast yapoteza dhidi ya Ujerumani dakika za jioni
Ivory Coast yapoteza dhidi ya Ujerumani dakika za jioni
Today, READ MORE β†’
Real Madrid yakana kuwasiliana na Olise, wakala wake
Real Madrid yakana kuwasiliana na Olise, wakala wake
Yesterday, READ MORE β†’
Simba 4-0 Coastal Union, CRDB Cup
Simba 4-0 Coastal Union, CRDB Cup
Yesterday, READ MORE β†’
Simba yaifumua Coastal Union 4-0, yatinga fainali ya CRDB Bank Cup
Simba yaifumua Coastal Union 4-0, yatinga fainali ya CRDB Bank Cup
Yesterday, READ MORE β†’