Local,Normal News,Azam Fc, Mali

Ibenge ajiondoa mchakato wa uteuzi wa kocha Mali

Joel JJ By Joel JJ
2 Jun 2026
Ibenge ajiondoa mchakato wa uteuzi wa kocha Mali

Kocha Mkuu wa Azam Fc, Jean-Florent Ibenge, hatakuwa kocha mpya wa timu ya taifa ya Mali baada ya kujiondoa katika mchakato wa uteuzi akiwa hatua za mwisho kabisa.

Taarifa kutoka Shirikisho la Soka la Mali, Fédération Malienne de Football (FEMAFOOT), zimeeleza kuwa Ibenge alikuwa ameshafikia hatua ya juu katika mazungumzo na hata kuchaguliwa kama mgombea namba moja kwa ajili ya kuchukua mikoba ya timu ya taifa, maarufu kama “The Eagles”.

Hata hivyo, ghafla kocha huyo ameamua kujiondoa kwenye mchakato huo akitaja sababu za kifamilia zilizopelekea kushindwa kuendelea na majukumu hayo mapya. Uamuzi huo umeibua mshangao mkubwa ndani ya uongozi wa soka nchini Mali, hasa kwa kuwa mchakato ulikuwa umefikia hatua ya mwisho kabisa.

Kwa mujibu wa taarifa hizo, viongozi wa FEMAFOOT wamesikitishwa na hatua hiyo wakiamini kuwa muda muhimu umepotea katika kipindi ambacho walitarajia kumtangaza kocha mpya. Baadhi ya maafisa wanahisi kwamba kama changamoto za kifamilia zilikuwepo, Ibenge alipaswa kuzibainisha mapema kabla ya kufikia hatua ya makubaliano ya juu.

Inaelezwa kuwa Ibenge alipitia hatua zote za usaili na tathmini, na alikuwa amepitishwa kama chaguo bora la kuinoa Mali, lakini alitoa taarifa ya kujiondoa wakati mazungumzo yakiwa yamekaribia kukamilika.

Kwa sasa, Shirikisho la Soka la Mali linaendelea tena na mchakato wa kutafuta kocha mpya, huku likilazimika kurejea orodha ya wagombea wengine waliokuwa wamepita awali. 

Inaelezwa Azam Fc imepiga hatua kubwa kumshawishi Ibenge na huenda akaongeza mkataba kuendelea kuinoa Azam Fc.

More Stories

APR Fc yawaondosha aigles du congo kwenye caf champions league
APR Fc yawaondosha aigles du congo kwenye caf champions league
6h ago
READ MORE →
Azam Fc yaomboleza kifo cha mlinda lango U20
Azam Fc yaomboleza kifo cha mlinda lango U20
10h ago
READ MORE →
Hatuna presha kuikabili Yanga - Kocha Gaborone United
Hatuna presha kuikabili Yanga - Kocha Gaborone United
11h ago
READ MORE →
Manqoba aweka tahadhari mechi dhidi ya Gaborone United
Manqoba aweka tahadhari mechi dhidi ya Gaborone United
13h ago
READ MORE →
Rasmi: João Pedro Atwaa Tuzo Ya Mchezaji Bora Wa Mwezi Wa Agosti
Rasmi: João Pedro Atwaa Tuzo Ya Mchezaji Bora Wa Mwezi Wa Agosti
16h ago
READ MORE →
Simba inalenga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, nusu fainali ni lengo kubwa
Simba inalenga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, nusu fainali ni lengo kubwa
16h ago
READ MORE →
Libasse awapiga chini Max na Mwajanga, Kwenye tuzo za Mwezi.
Libasse awapiga chini Max na Mwajanga, Kwenye tuzo za Mwezi.
16h ago
READ MORE →
Fei Toto azipotezea Simba, Yanga
Fei Toto azipotezea Simba, Yanga
18h ago
READ MORE →
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 21, Septemba 11 2026
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 21, Septemba 11 2026
22h ago
READ MORE →
UEFA champions league: matokeo ya usiku
UEFA champions league: matokeo ya usiku
1d ago
READ MORE →