Ibenge ajiondoa mchakato wa uteuzi wa kocha Mali

Joel JJ By Joel JJ • 2nd June 2026


Ibenge ajiondoa mchakato wa uteuzi wa kocha Mali

Kocha Mkuu wa Azam Fc, Jean-Florent Ibenge, hatakuwa kocha mpya wa timu ya taifa ya Mali baada ya kujiondoa katika mchakato wa uteuzi akiwa hatua za mwisho kabisa.

Taarifa kutoka Shirikisho la Soka la Mali, Fédération Malienne de Football (FEMAFOOT), zimeeleza kuwa Ibenge alikuwa ameshafikia hatua ya juu katika mazungumzo na hata kuchaguliwa kama mgombea namba moja kwa ajili ya kuchukua mikoba ya timu ya taifa, maarufu kama “The Eagles”.

Hata hivyo, ghafla kocha huyo ameamua kujiondoa kwenye mchakato huo akitaja sababu za kifamilia zilizopelekea kushindwa kuendelea na majukumu hayo mapya. Uamuzi huo umeibua mshangao mkubwa ndani ya uongozi wa soka nchini Mali, hasa kwa kuwa mchakato ulikuwa umefikia hatua ya mwisho kabisa.

Kwa mujibu wa taarifa hizo, viongozi wa FEMAFOOT wamesikitishwa na hatua hiyo wakiamini kuwa muda muhimu umepotea katika kipindi ambacho walitarajia kumtangaza kocha mpya. Baadhi ya maafisa wanahisi kwamba kama changamoto za kifamilia zilikuwepo, Ibenge alipaswa kuzibainisha mapema kabla ya kufikia hatua ya makubaliano ya juu.

Inaelezwa kuwa Ibenge alipitia hatua zote za usaili na tathmini, na alikuwa amepitishwa kama chaguo bora la kuinoa Mali, lakini alitoa taarifa ya kujiondoa wakati mazungumzo yakiwa yamekaribia kukamilika.

Kwa sasa, Shirikisho la Soka la Mali linaendelea tena na mchakato wa kutafuta kocha mpya, huku likilazimika kurejea orodha ya wagombea wengine waliokuwa wamepita awali. 

Inaelezwa Azam Fc imepiga hatua kubwa kumshawishi Ibenge na huenda akaongeza mkataba kuendelea kuinoa Azam Fc.


  

More Stories

Azam Fc hiyooo fainali, yaichapa Yanga 3-2 nusu fainali
Azam Fc hiyooo fainali, yaichapa Yanga 3-2 nusu fainali
Today, READ MORE →
Azam Fc 3-2 Yanga, CRDB Cup
Azam Fc 3-2 Yanga, CRDB Cup
Today, READ MORE →
Ni Azam Fc vs Yanga, nani anakwenda fainali kombe la CRDB?
Ni Azam Fc vs Yanga, nani anakwenda fainali kombe la CRDB?
Today, READ MORE →
Liverpool kuongeza dau kumnasa Diomande
Liverpool kuongeza dau kumnasa Diomande
Today, READ MORE →
Prisons wamefufua matumaini kusalia ligi kuu
Prisons wamefufua matumaini kusalia ligi kuu
Today, READ MORE →
Tunisia yaaga kombe la Dunia kwa aibu, yapigwa 4-0 na Japan
Tunisia yaaga kombe la Dunia kwa aibu, yapigwa 4-0 na Japan
Today, READ MORE →
Ivory Coast yapoteza dhidi ya Ujerumani dakika za jioni
Ivory Coast yapoteza dhidi ya Ujerumani dakika za jioni
Today, READ MORE →
Real Madrid yakana kuwasiliana na Olise, wakala wake
Real Madrid yakana kuwasiliana na Olise, wakala wake
Yesterday, READ MORE →
Simba 4-0 Coastal Union, CRDB Cup
Simba 4-0 Coastal Union, CRDB Cup
Yesterday, READ MORE →
Simba yaifumua Coastal Union 4-0, yatinga fainali ya CRDB Bank Cup
Simba yaifumua Coastal Union 4-0, yatinga fainali ya CRDB Bank Cup
Yesterday, READ MORE →