Beki wa kati wa kimataifa wa Ufaransa, Ibrahima Konaté, ameripotiwa kufikia makubaliano ya awali kujiunga na miamba wa Hispania, Real Madrid, katika mkataba wa miaka minne kama mchezaji huru.
Kwa mujibu wa taarifa, Konaté ameondoka rasmi katika klabu ya Liverpool FC baada ya mkataba wake kumalizika, na amechagua kuanza ukurasa mpya katika dimba la Santiago Bernabéu.





