Local,Normal News,Yanga

Pacome, Zimbwe Jr waongeza nguvu Yanga

Joel JJ By Joel JJ
2 Jun 2026
Pacome, Zimbwe Jr waongeza nguvu Yanga

Klabu ya Yanga SC imepokea boost kubwa kuelekea mechi za mwisho wa msimu baada ya wachezaji wake muhimu, Pacome Zouzoua na Mohamed Hussein ‘Zimbwe Jr’, kurejea kikosini na kuanza mazoezi kikamilifu.

Kiungo mshambuliaji raia wa Ivory Coast, Pacôme Zouzoua, alikuwa miongoni mwa wachezaji waliorejea mazoezini jana katika kituo cha KMC Complex, akianza tena maandalizi ya mechi zilizobaki baada ya kuwa nje kwa muda kutokana na majeraha ya goti.

Pacome alipata majeraha hayo katika mchezo dhidi ya Singida Black Stars, hali iliyomfanya akose baadhi ya mechi muhimu kabla ya mapumziko ya kalenda ya FIFA. Hata hivyo, sasa amerejea akiwa fiti na kushiriki kikamilifu katika program za mazoezi chini ya benchi la ufundi.

Urejeo wake unatajwa kuwa muhimu sana kwa Yanga SC, ambayo inaendelea kupambana kutetea ubingwa wa Ligi Kuu Tanzania Bara pamoja na kushiriki mechi ngumu za mashindano ya Kombe la CRDB.

Katika upande mwingine, beki wa kushoto wa Yanga, Mohamed Hussein Zimbwe Jr, naye amerejea kikosini baada ya kuwa nje kwa wiki kadhaa akiuguza majeraha. Sasa ameonekana akiwa fiti na kushiriki mazoezi yote pamoja na wenzake.

Uwepo wa Zimbwe Jr unatoa nafuu kubwa kwa kikosi cha Yanga, hasa katika eneo la ulinzi wa pembeni, ambapo uzoefu wake unahitajika katika mechi muhimu zinazokuja.

Mazoezi ya Yanga yameendelea ambapo jana na leo wachezaji wamefanya session mbili tofauti. Asubuhi walipitia programu maalum ya mazoezi ya gym, kabla ya mchana kuendelea na mazoezi ya uwanjani chini ya makocha Abdihamid Moalin na Patrick Mabedi.

More Stories

Barcelona yaendeleza kichapo Laliga ikimfunga Sevilla, Raphinha hashikiki.
Barcelona yaendeleza kichapo Laliga ikimfunga Sevilla, Raphinha hashikiki.
3h ago
READ MORE →
Mamelodi Sundowns yaibuka kidedea mbele ya Al Ahli
Mamelodi Sundowns yaibuka kidedea mbele ya Al Ahli
7h ago
READ MORE →
Arsenal yaduwazwa 3-0 na Brighton
Arsenal yaduwazwa 3-0 na Brighton
8h ago
READ MORE →
Nyota Stars waingia kambini tayari kwa mechi za kufuzu Afcon 2027
Nyota Stars waingia kambini tayari kwa mechi za kufuzu Afcon 2027
10h ago
READ MORE →
Simba kujichimbia Afrika Kusini kujiandaa na Kariakoo Derby
Simba kujichimbia Afrika Kusini kujiandaa na Kariakoo Derby
10h ago
READ MORE →
Madrid Derby: Atletico na Real kwenye vita ya majirani
Madrid Derby: Atletico na Real kwenye vita ya majirani
14h ago
READ MORE →
Hii hapa rekodi tamu ya Barker Ligi Kuu
Hii hapa rekodi tamu ya Barker Ligi Kuu
16h ago
READ MORE →
Sundowns kuchuana na Al Ahli katika vita ya Afrika na Asia
Sundowns kuchuana na Al Ahli katika vita ya Afrika na Asia
17h ago
READ MORE →
Ft: Yanga 1-0 St George, Yanga yapata ushindi mechi ya kirafiki.
Ft: Yanga 1-0 St George, Yanga yapata ushindi mechi ya kirafiki.
1d ago
READ MORE →
Dockers Derby yarudi baada ya miaka 14, Ulinzi wa London ukiimarishwa.
Dockers Derby yarudi baada ya miaka 14, Ulinzi wa London ukiimarishwa.
1d ago
READ MORE →