Pacome, Zimbwe Jr waongeza nguvu Yanga

Joel JJ By Joel JJ • 2nd June 2026


Pacome, Zimbwe Jr waongeza nguvu Yanga

Klabu ya Yanga SC imepokea boost kubwa kuelekea mechi za mwisho wa msimu baada ya wachezaji wake muhimu, Pacome Zouzoua na Mohamed Hussein ‘Zimbwe Jr’, kurejea kikosini na kuanza mazoezi kikamilifu.

Kiungo mshambuliaji raia wa Ivory Coast, Pacôme Zouzoua, alikuwa miongoni mwa wachezaji waliorejea mazoezini jana katika kituo cha KMC Complex, akianza tena maandalizi ya mechi zilizobaki baada ya kuwa nje kwa muda kutokana na majeraha ya goti.

Pacome alipata majeraha hayo katika mchezo dhidi ya Singida Black Stars, hali iliyomfanya akose baadhi ya mechi muhimu kabla ya mapumziko ya kalenda ya FIFA. Hata hivyo, sasa amerejea akiwa fiti na kushiriki kikamilifu katika program za mazoezi chini ya benchi la ufundi.

Urejeo wake unatajwa kuwa muhimu sana kwa Yanga SC, ambayo inaendelea kupambana kutetea ubingwa wa Ligi Kuu Tanzania Bara pamoja na kushiriki mechi ngumu za mashindano ya Kombe la CRDB.

Katika upande mwingine, beki wa kushoto wa Yanga, Mohamed Hussein Zimbwe Jr, naye amerejea kikosini baada ya kuwa nje kwa wiki kadhaa akiuguza majeraha. Sasa ameonekana akiwa fiti na kushiriki mazoezi yote pamoja na wenzake.

Uwepo wa Zimbwe Jr unatoa nafuu kubwa kwa kikosi cha Yanga, hasa katika eneo la ulinzi wa pembeni, ambapo uzoefu wake unahitajika katika mechi muhimu zinazokuja.

Mazoezi ya Yanga yameendelea ambapo jana na leo wachezaji wamefanya session mbili tofauti. Asubuhi walipitia programu maalum ya mazoezi ya gym, kabla ya mchana kuendelea na mazoezi ya uwanjani chini ya makocha Abdihamid Moalin na Patrick Mabedi.


  

More Stories

Azam Fc hiyooo fainali, yaichapa Yanga 3-2 nusu fainali
Azam Fc hiyooo fainali, yaichapa Yanga 3-2 nusu fainali
Today, READ MORE →
Azam Fc 3-2 Yanga, CRDB Cup
Azam Fc 3-2 Yanga, CRDB Cup
Today, READ MORE →
Ni Azam Fc vs Yanga, nani anakwenda fainali kombe la CRDB?
Ni Azam Fc vs Yanga, nani anakwenda fainali kombe la CRDB?
Today, READ MORE →
Liverpool kuongeza dau kumnasa Diomande
Liverpool kuongeza dau kumnasa Diomande
Today, READ MORE →
Prisons wamefufua matumaini kusalia ligi kuu
Prisons wamefufua matumaini kusalia ligi kuu
Today, READ MORE →
Tunisia yaaga kombe la Dunia kwa aibu, yapigwa 4-0 na Japan
Tunisia yaaga kombe la Dunia kwa aibu, yapigwa 4-0 na Japan
Today, READ MORE →
Ivory Coast yapoteza dhidi ya Ujerumani dakika za jioni
Ivory Coast yapoteza dhidi ya Ujerumani dakika za jioni
Today, READ MORE →
Real Madrid yakana kuwasiliana na Olise, wakala wake
Real Madrid yakana kuwasiliana na Olise, wakala wake
Yesterday, READ MORE →
Simba 4-0 Coastal Union, CRDB Cup
Simba 4-0 Coastal Union, CRDB Cup
Yesterday, READ MORE →
Simba yaifumua Coastal Union 4-0, yatinga fainali ya CRDB Bank Cup
Simba yaifumua Coastal Union 4-0, yatinga fainali ya CRDB Bank Cup
Yesterday, READ MORE →