International,Transfer News,Real Madrid, Inter Milan, Liverpool, Local

Mourinho aanza na Kounate, Dumfries

Joel JJ By Joel JJ
3 Jun 2026
Mourinho aanza na Kounate, Dumfries

Ripoti mpya kutoka vyanzo vya soka barani Ulaya zinaeleza kuwa kocha mtarajiwa wa Real Madrid José Mourinho amepitisha usajili wa beki wa Liverpool Ibrahima Konaté pamoja na beki wa pembeni wa Inter Milan Denzel Dumfries kujiunga na miamba hiyo ya Hispania baada ya mchakato wa uchaguzi wa uongozi ndani ya klabu kukamilika.

Inaelezwa kuwa tayari kuna mazungumzo ya awali yaliyofanyika na pande husika, na hata makubaliano ya maneno (verbal agreements) yanadaiwa kufikiwa kwa baadhi ya vipengele vya usajili. 

Kwa mujibu wa nguli wa habari za usajili Fabrizio Romano, nyota hao watajiunga na Real Madrid baada ya taratibu za uchaguzi ndani ya klabu hiyo kukamilika.

Mourinho ameanza kwa kuisuka upya safu ya ulinzi. Konaté anatajwa kwa uwezo wake eneo la beki wa kati, uongozi na nguvu katika kuzuia mashambulizi, huku Dumfries akiwa na kasi na mchango mkubwa katika kushambulia kutoka pembeni.

More Stories

Barcelona yaendeleza kichapo Laliga ikimfunga Sevilla, Raphinha hashikiki.
Barcelona yaendeleza kichapo Laliga ikimfunga Sevilla, Raphinha hashikiki.
2h ago
READ MORE →
Mamelodi Sundowns yaibuka kidedea mbele ya Al Ahli
Mamelodi Sundowns yaibuka kidedea mbele ya Al Ahli
6h ago
READ MORE →
Arsenal yaduwazwa 3-0 na Brighton
Arsenal yaduwazwa 3-0 na Brighton
7h ago
READ MORE →
Nyota Stars waingia kambini tayari kwa mechi za kufuzu Afcon 2027
Nyota Stars waingia kambini tayari kwa mechi za kufuzu Afcon 2027
9h ago
READ MORE →
Simba kujichimbia Afrika Kusini kujiandaa na Kariakoo Derby
Simba kujichimbia Afrika Kusini kujiandaa na Kariakoo Derby
9h ago
READ MORE →
Madrid Derby: Atletico na Real kwenye vita ya majirani
Madrid Derby: Atletico na Real kwenye vita ya majirani
13h ago
READ MORE →
Hii hapa rekodi tamu ya Barker Ligi Kuu
Hii hapa rekodi tamu ya Barker Ligi Kuu
15h ago
READ MORE →
Sundowns kuchuana na Al Ahli katika vita ya Afrika na Asia
Sundowns kuchuana na Al Ahli katika vita ya Afrika na Asia
15h ago
READ MORE →
Ft: Yanga 1-0 St George, Yanga yapata ushindi mechi ya kirafiki.
Ft: Yanga 1-0 St George, Yanga yapata ushindi mechi ya kirafiki.
1d ago
READ MORE →
Dockers Derby yarudi baada ya miaka 14, Ulinzi wa London ukiimarishwa.
Dockers Derby yarudi baada ya miaka 14, Ulinzi wa London ukiimarishwa.
1d ago
READ MORE →