International,Transfer News,Manchester United, Inter, Local

Ederson kutua Manchester United

Joel JJ By Joel JJ
3 Jun 2026
Ederson kutua Manchester United

Kiungo wa Atlanta Ederson amekamilisha uhamisho wake wa kujiunga na Manchester United katika dili linalofikia thamani ya takriban €45 milioni pamoja na nyongeza (add-ons).

Makubaliano kati ya klabu hizo mbili yamekamilika baada ya mazungumzo yaliyodumu kwa wiki kadhaa, huku dili likifungwa rasmi na sasa kinachosubiriwa ni hatua za mwisho za kimatibabu (medical tests) na taratibu za usajili kabla ya tangazo rasmi kutolewa.

Usajili wa Kwanza wa Carrick

Inaripotiwa kuwa Éderson atakuwa usajili wa kwanza wa kocha mpya wa Manchester United, Michael Carrick, katika dirisha hili la majira ya joto, ikiwa ni sehemu ya mpango wa kuijenga upya timu hiyo kwa msimu ujao.

Carrick anaelezwa kuwa na mpango wa kuimarisha eneo la kiungo kwa kuongeza nguvu, uimara na ubunifu, na Éderson anaonekana kuwa chaguo sahihi kutokana na uwezo wake wa kukaba, kupandisha mashambulizi na kudhibiti tempo ya mchezo.

Vyanzo vya karibu na dili hilo vinasema kuwa mazungumzo kati ya Manchester United na Atalanta yalikuwa yameingia hatua za mwisho kwa muda, na sasa kila kitu kimekamilika kwa pande zote mbili. Mkataba wa miaka minne umekubaliwa kati ya mchezaji na klabu mpya.

More Stories

Barcelona yaendeleza kichapo Laliga ikimfunga Sevilla, Raphinha hashikiki.
Barcelona yaendeleza kichapo Laliga ikimfunga Sevilla, Raphinha hashikiki.
6h ago
READ MORE →
Mamelodi Sundowns yaibuka kidedea mbele ya Al Ahli
Mamelodi Sundowns yaibuka kidedea mbele ya Al Ahli
11h ago
READ MORE →
Arsenal yaduwazwa 3-0 na Brighton
Arsenal yaduwazwa 3-0 na Brighton
11h ago
READ MORE →
Nyota Stars waingia kambini tayari kwa mechi za kufuzu Afcon 2027
Nyota Stars waingia kambini tayari kwa mechi za kufuzu Afcon 2027
13h ago
READ MORE →
Simba kujichimbia Afrika Kusini kujiandaa na Kariakoo Derby
Simba kujichimbia Afrika Kusini kujiandaa na Kariakoo Derby
14h ago
READ MORE →
Madrid Derby: Atletico na Real kwenye vita ya majirani
Madrid Derby: Atletico na Real kwenye vita ya majirani
17h ago
READ MORE →
Hii hapa rekodi tamu ya Barker Ligi Kuu
Hii hapa rekodi tamu ya Barker Ligi Kuu
19h ago
READ MORE →
Sundowns kuchuana na Al Ahli katika vita ya Afrika na Asia
Sundowns kuchuana na Al Ahli katika vita ya Afrika na Asia
20h ago
READ MORE →
Ft: Yanga 1-0 St George, Yanga yapata ushindi mechi ya kirafiki.
Ft: Yanga 1-0 St George, Yanga yapata ushindi mechi ya kirafiki.
1d ago
READ MORE →
Dockers Derby yarudi baada ya miaka 14, Ulinzi wa London ukiimarishwa.
Dockers Derby yarudi baada ya miaka 14, Ulinzi wa London ukiimarishwa.
1d ago
READ MORE →