Local,Transfer News,Yanga, Marumo, Kabylie

Yanga yaanza mikakati ya kusukwa upya

Joel JJ By Joel JJ
β€’
4 Jun 2026
Yanga yaanza mikakati ya kusukwa upya

Wakati mashabiki wa Yanga SC wakiendelea kusubiri hitimisho la msimu huu, uongozi wa klabu hiyo tayari umeanza maandalizi ya awali ya kusuka upya kikosi kitakachoshiriki msimu ujao wa mashindano ya ndani na kimataifa.

Taarifa kutoka ndani ya klabu hiyo zinaeleza kuwa mabingwa hao wa Tanzania Bara wameanza michakato ya awali ya usajili, wakilenga kufanya maboresho makubwa zaidi ili kuhakikisha kila nafasi muhimu inapata mchezaji mwenye ubora unaotakiwa.

Baada ya kutofanya vyema katika dirisha kubwa la usajili lililopita, safari hii Yanga imepanga kuingia sokoni kwa umakini mkubwa zaidi, ikiwa na mpango wa kuhakikisha kila usajili unakuwa na tija kwa kikosi cha benchi la ufundi.

Chanzo kutoka ndani ya uongozi kimeeleza kuwa klabu hiyo inatarajia kufanya mabadiliko makubwa katika idara ya wachezaji wa kigeni, ambapo nyota wasiopungua saba wanatajwa kuwa kwenye mipango ya kutua Jangwani mara dirisha la usajili litakapofunguliwa rasmi.

Iwapo mpango huo utatekelezwa kama ulivyopangwa, itamaanisha kuwa kati ya wachezaji 12 wa kigeni waliopo kwa sasa, ni watano pekee watakaosalia ndani ya kikosi cha msimu ujao, huku wengine wakitarajiwa kuachana na klabu hiyo kutokana na sababu mbalimbali ikiwemo kumaliza mikataba au kutokuwa kwenye mipango ya benchi la ufundi.

Kwa sasa, Yanga tayari imeanza mchakato wa kusafisha kikosi chake kwa kuachana na baadhi ya wachezaji waliokuwa wametolewa kwa mkopo katika klabu mbalimbali. Taarifa zinaeleza kuwa kiungo Mohamed Doumbia, Celestin Ecua, Jonathan Ikangalombo pamoja na Moussa Balla Conte hawatakuwa sehemu ya mipango ya Yanga msimu ujao, baada ya uongozi kuamua kutoendelea nao.

Mbali na wachezaji hao waliokuwa kwa mkopo, benchi la ufundi pia linatarajiwa kufanya tathmini ya mwisho kwa baadhi ya nyota waliopo kikosini kwa sasa. Wale ambao hawataingia kwenye mipango ya msimu ujao wataachwa ili kupisha usajili mpya.

More Stories

Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
1h ago
READ MORE β†’
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
1h ago
READ MORE β†’
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
2h ago
READ MORE β†’
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
3h ago
READ MORE β†’
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
3h ago
READ MORE β†’
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
4h ago
READ MORE β†’
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
5h ago
READ MORE β†’
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
18h ago
READ MORE β†’
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
18h ago
READ MORE β†’
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
19h ago
READ MORE β†’