Local,Transfer News,Tetesi, Yanga

Yanga yarudi kwa Dala

Joel JJ By Joel JJ
β€’
5 Jun 2026
Yanga yarudi kwa Dala

Yanga wamehuisha tena mpango wao wa kumsajili winga wa kimataifa wa Angola, Gelson Dala, kuelekea dirisha kubwa la usajili linalotarajiwa kufunguliwa mwezi ujao.

Katika dirisha dogo la usajili lililopita, Yanga ilifanya juhudi kubwa kumleta Dala kutoka klabu ya Qatar ya Al Wakrah SC, lakini mpango huo haukufanikiwa baada ya changamoto za uhamisho wake.

Kwa mujibu wa taarifa, Yanga ilikuwa imepanga kufanya usajili wa pamoja wa Dala na Laurindo Aurelio β€œDepu”, lakini ilifanikiwa kumsajili Depu pekee, huku Dala akibaki katika klabu yake ya Qatar.

Baada ya kushindikana kwa mpango huo, mabingwa hao wa Tanzania Bara waliendelea kuimarisha kikosi chao kwa kumsajili Buba Jammeh katika hatua za mwisho za dirisha dogo, usajili ambao ulipendekezwa na aliyekuwa kocha wa timu hiyo, Pedro Goncalves.

Goncalves, kocha wa zamani wa Yanga, alikuwa ameweka wazi kuwataka wachezaji wote wawili, Dala na Depu, kutokana na uzoefu wake nao akiwa kwenye timu ya taifa ya Angola.

Sasa taarifa mpya zinaeleza kuwa Yanga bado haijakata tamaa, na mpango wa kumsajili Dala upo palepale, ambapo kuna uwezekano mkubwa wa mchezaji huyo kujiunga na klabu hiyo katika dirisha lijalo la usajili.

Inaelezwa kuwa Yanga na Dala walikuwa tayari wamefikia makubaliano ya awali, lakini dili hilo lilikwama kutokana na klabu yake ya Al Wakrah kutokuwa tayari kumruhusu kuondoka wakati wa dirisha dogo.

Endapo mazungumzo yatakamilika kwa mafanikio, Dala anaweza kuwa moja ya usajili mkubwa kwa timu hiyo katika kujiandaa na msimu mpya wa mashindano ya ndani na kimataifa.

More Stories

Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
9m ago
READ MORE β†’
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
38m ago
READ MORE β†’
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
1h ago
READ MORE β†’
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
2h ago
READ MORE β†’
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
2h ago
READ MORE β†’
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
3h ago
READ MORE β†’
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
3h ago
READ MORE β†’
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
16h ago
READ MORE β†’
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
17h ago
READ MORE β†’
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
18h ago
READ MORE β†’